Umoja wa Wamama Wakuu TZ wajenga ofisi mpya Tegeta




NA PHILIPO JOSEPHAT DSM
UMOJA wa Wamama Wakuu Tanzania (TCAS) umejenga ofisi mpya Tegeta jijini Dar es Salaam na kufunguliwa rasmi Novemba 9 mwaka huu na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.
Akifungua jengo hilo, Kardinali Pengo amewapongeza watawa kwa hatua hiyo huku akiwatakia heri kwa kazi ambayo Mungu ameianzisha na aifikishe kulingana  na baraka alizozitoa.
“Mipango ya Mwenyezi Mungu  kamwe haishindwi, kwa sababu ni yeye anayebariki kila lililo jema. Jambo la msingi ni kuhakikisha mnaimarisha umoja wenu kwakuwa ninyi ni wamoja,” amesema Kardinali Pengo.
Aidha mewasisitiza kuwa na ukaribu na Jimbo Kuu  Katoliki Dar es salaam .
Akizungumza katika tukio hilo, Mwenyekiti wa Umoja wa Wamama Wakuu Tanzania Sista Gaspara Kashamba ambaye ametoka Shirika la Masista wa Usambara Jimbo Katoliki Tanga amewashukuru  Maaskofu wote kwa kuwachangia na kufanikisha ujenzi wa ofisi hiyo, Wamama Wakuu kwa juhudi za kujinyima na kujali umoja wao kwa kutoa michango bila kuwasahau wakandarasi waliojenga ofisi hiyo.
Amesema nyumba mpya itatumika kama ofisi ya (TCAS), na malengo yao kwa sasa ni kuhakikisha wanajenga ukumbi na hosteli ya kulala watu.

Kwa upande wake Katibu wa umoja huo Sista Claudia Mashambo, amemshukuru Mungu kwa kuwapatia ofisi, jambo litakalopanua wigo wa utumishi wao, kwa kufanya kazi za utumishi kwa ufanisi mkubwa, huku wakiendelea na mipango ya kujenga hosteli na ukumbi.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU