Mama Janeth Magufuli atoa msaada kwa wazee Tabora

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Awamu ya tano Mama Janeth Magufuli ametoa msaada wa vyakula na vitu mbalimbali kwa wazee na walemavu katika kijiji cha Amani Ipuli Tabora na kuwaomba wanatabora kuwa na moyo wa huruma kwa wazee na wahitaji.
Mama Janeth ametoa unga wa mahindi kilo 3521, mchele kilo 3125, maharage kilo 1250, mafuta ya kula , sabuni za kufulia, mafuta maalumu ya kupaka kwa watoto walemavu wa ngozi na vitu vingine muhimu kwa wazee wa kituo hicho.
Pia ametoa msaada wa vitu mbalimbali katika gereza la Mahabusu Tabora maarufu kama gereza la Zuberi.
Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora Dr. Tea Ntara  amemuhakikishia Mama Janeth kuwa serikali ya mkoa imejipanga vizuri na hivyo misaada yote itawafikia kwa utaratibu na hakuna kitu kitakachopotea.
Wakati huo huo Mbuge wa Tabora mjini kupitia viti maalumu (CCM) Mwanne mchemba amemhakikishia Mama Janeth kuwa Chama Cha Mapinduzi kinaunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais Dr. John Pombe Magufuli  dhidi ya vita vya dawa za kulevya ambazo zinayoharibu vijana na Taifa hili.
Naye Afisa Ustawi wa Jamii Manispaa Tabora Baraka alitoa baadhi ya changamoto zinazokikumba kituo hicho cha wazee cha Amani, Ipuli na Tabora kuwa ni ukosefu wa usafiri, uchakafu wa majengo, vyoo vya kudumu na mabafu, upungufu wa wahudumu, uvamizi wa maeneo ya kijiji hicho na mavazi kwa wazee wanaoishi mahali hapo.
Mama Janeth Magufuli alifuatana na Mama Merry Majaliwa mke wa Mh . Waziri Mkuu  wote kwa pamoja wakiwahimiza  wananchi kuwa na moyo wa ukarimu kwa watu wenye shida.
Shughuli hiyo ya kutoa msaada kwa wazee na watu wenyeshida ilihudhuriwa na Naibu Waziri wa Afya na Mbunge wa Jimbo la Nzega Mh Hamis Kigwangala, Viongozi wa Serikali, Viongozi wa vyama vya siasa,  viongozi wa Dini na wanainchi wa manispaa ya Tabora.
Kituo hicho kilianzishwa mwaka 1969 kama kituo cha kulea wazee waliokuwa wametengwa na ndugu zao baada ya kupata ugonjwa wa ukoma sasa kipo rasmi chini ya Uangalizi wa Manispaa ukipokea watu wote waliotengwa na jamii zao.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU