Padri akemea watoto kuvalishwa hirizi

WAAMINI wameonywa kutojihusisha na imani potofu kwa kuwavalisha watoto wao hirizi na vitu visivyokubalika mbele za Mwenyezi Mungu.
Onyo hilo limetolewa na Padri Wanyonyi Simiyuss kwenye ibada ya kuwabatiza watoto iliyofanyika katika Parokia hiyo ambapo amewataka waamini kuachana na tabia hiyo ya kuwavalisha watoto hirizi.
Amesema kuwa Mungu mwenyewe hakubaliani na hilo kwa kuwa suala hilo linaashiria kuwa ni la kishirikina na linakubaliwa na shetani mwenyewe.
Amesema kuwa kitendo cha kuwavalisha watoto wadogo hirizi na vitu vinginevyo visivyokubalika mbele za Mungu ni ishara kubwa inayoonyesha kushiriki ibada za kishirikina za kishetani ambazo hazina nafasi kwa watoto hao ambao ni wadogo.
“Kitendo hicho cha kuwavalisha hirizi na shanga ambazo hazina maana yoyote mbele za Mungu, sitokubaliana na jambo hilo na kila nitakapofanya ibada ya kuwabatiza watoto itabidi nifanye kwanza uchunguzi na kama watabainika sitohusika na dhambi hiyo.”Amesema.
Hata hivyo amewataka waamini hao kumtolea Mwenyezi Mungu zabihu iliyonona ili waweze kubarikiwa ikizingatiwa kuwa ni agizo na lipo kwenye maandiko ya Biblia.
Amesema haipendezi kuona wakristo haohao wanatoa vitu vyenye thamani kubwa kwenye sherehe kama vile za ndoa, kicheni pati na kumbukumbu ya kuzaliwa, lakini linapofikia suala ya kumtolea Mungu hawafanyi kama huko kwingine.
“Harusi, kicheni pati kumbukumbu ya kuzaliwa vitu hivyo waamini wapo mstari wa mbele katika kuchangia, lakini suala la kumtolea Mungu zabihu iliyonona ni vigumu kwao hii kwa kweli inasikitisha tena ni dhambi na mnatakiwa kutubu tu,”amesema.
Padri huyo pia amewataka wasimamizi wa watoto waliobatizwa kwenye ibada hiyo kuhakikisha shetani hawatumii katika vitendo viovu, bali kinachotakiwa wawape malezi bora na misingi ya kiroho itakayowafanya kumpenda Mungu wao.

Amesema jukumu la kuhakikisha watoto hao wanapata malezi hayo pia lipo kwao kwa kushirikiana na wazazi wao ambapo kwa kufanya hivyo taifa litaweza kuwapata viongozi ambao watakakuwa wacha Mungu na waadirifu kwa serikali.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU