‘Hakuna maendeleo bila Kanisa’ Mwinyi asema

RAIS Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awamu ya pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi amesema kuwa Kanisa ni chombo muhimu katika maendeleo ya jamii ya Tanzania, hasa kwa kuchangia katika kuweka mazingira chanya ya upatikanaji wa elimu na afya.
Alhaji Mwinyi ameeleza hayo katika maadhimisho ya jubilei ya miaka 25 ya Tume ya Kikristo ya Huduma za Jamii nchini (CSSC), yaliyofanyika jijini Dar es salaam hivi karibuni, ambapo amesema kuwa Kanisa daima liko mstari wambele katika katika kutoa huduma bora za elimu na afya nchini.
“Mara zote huwa nawaambia jamaa zangu kule Temeke, nendeni katika hospitali za Kanisa. Wale wenzetu wanafanya ile kazi kama sehemu ya ibada yao. Nawaambia wazi wakienda huko watapata dawa na upendo” amesema Mwinyi.
Ameongeza kuwa kutokana na ushirikiano huo baina ya makanisa nchini katika utoaji wa huduma, watanzania wengi wamepata huduma bora, na kuwaomba maaskofu waendelee kuithamini CSSC ili iendelee kustawi.
Ameweka wazi kuwa jamii ya watanzania inahitaji zaidi uwepo wa CSSC hivyo ametoa wito kwa viongozi wa tume hiyo kuendelea kupanua na kuboresha huduma za jamii.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU