“WATAWA MJIDHATITI KUJENGA MAHUSIANO KATI YENU, MAASKOFU, KANISA”

n  Na Sarah Pelaji, Dar es Salaam

WIto umetolewa kwa watawa wa kike kutoka kanda ya Afrika Mashariki na kati kuishi maisha yao ya wakfu kwa umojana maaskofu, mapadri, ndani ya jumuiya zao na jamii inayowazunguka.
Hayo yamebainishwa na Mwadhama  João Kardinali Bráz de Aviz, Rais wa Baraza la Kipapa la Maisha ya waliowekwa wakfu (CICLSAL) katika Mkutano Mkuu wa 17 wa Umoja wa Watawa wanawake Afrika Mashariki na kati uliofanyika katika Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Kurasini jijini Dar es Salaam kuanzia August 27-31 mwaka huu.
“Kusanyiko hili la watawa ni fursa yetu sote kuwa pamoja, kushirikishana karama zetu, changamoto zetu ili tukuwe pamoja kama wawekwa wakfu katika Kanisa.
Kardinali Bráz de Aviz ambaye awali alifungua mkutano huo kwa Ibada ya Misa Takatifu alitaka watawa waangalie changamoto zao za sasa kama wanajiandaaje na kuishi maisha mapya baada ya mkutano huo kwani wato wa Baba Mtakatifu Fransisko kwa watawa na kwa Kanisa ni kujitakatifuza kwa kufanya mang’amuzi mapya ya maisha ya wakfu,” amesisistiza Karidinal Bráz de Aviz.
Amewataka watawa watathmini mahusiano yao na viongozi wa Kanisa hususani Maaskofu na wote wenye mamlaka katika Kanisa akiwataka warejee waraka wa Iuvenescit Ecclesia  uliotolewa na Kongrigasio ya uenezaji Injili.
“Baba Mtakatifu amesisitiza kongrigasio ya CICLSAL na kongrigasio ya Maaskofu kupitia na kufanya marejeo ya waraka wa Mutae relationes’ (Mutual Relations).
Nyaraka zote mbili zinazungumzia mahusiano thabiti kati ya Maaskofu na watawa (wawekwa wakfu) kwa ajili ya kujenga umoja katika maisha ya kiroho, kushirikishana karama  ili kuliendeleza Kanisa,” amesisitiza.
Amesema ni wakati mwafaka wa kufanya tathmini kuanzia mtu binafsi, jumuiya , shirika na umoja wa mashirika kuanza maisha mapya bila woga ili kuendeleza karama zao muhimu ndani ya Kanisa.
“Zipo baadhi ya changamoto ambazo zimo ndani ya jumuiya za watawa ikiwemo utengano. Utakuta baadhi ya watawa wanaunganika huku wakimtenga mtawa mmoja ndani ya jumuiya ambaye anabaki mpweke.
Inawezekana wakaenda hata safari na kufanya shughuli zao na kumwacha mtawa mmoja akiteseka kisaikolojia ndani ya jumuiya. Hii inaweza kumfanya akate tamaa, kusononeka na kutopata mazingira chanya ya kuishi wito wake wa utawa.
Ndiyo maana ninasisitiza umoja ndani ya jumuiya zetu za kitawa ili kuunganisha karama zenu na kuishi kwa furaha maisha ya kumtumikia Kristo,” amesema Kardinali huyo.
Kardinali de Aviz ameeleza changamoto nyingine ya watawa kuacha ,maisha ya wakfu akisema si jambo la kuchukuliwa kawaida bali jitihada ziwekwe na wakuu wa mashirika kuanzia ngazi za kitaifa na kimataifa.
“Walezi lazima wawe makini kutoa malezi yanayoheshimu na kuthamini mila na desturi mbalimbali za vjana pamoja na upana wa maisha ya kizazi cha sasa.
Kama hakuna uwiano kati ya teolojia na utaalmu katika mafunzo matokeo yake ni kukosa malezi yakini, nidhamu na maisha ya wakfu.
Lazima wanaolea yaani walezi wawe na malezi na utaalamupamoja na teolojia ya kulea wengine. Mlezi awe na malezi endelevu ndipo awalee wengine. Kadhalika wamama wakuu na uongozi mzima lazima wapate malezi endelevu ili kuweza kulea wanashirika.
Amesisitiza pia suala la utawala ndani ya mashirika ya wawekwa wakfu. Kuwe na majadiliano katika kuongoza mashirika ya kitawa ili kuwa na maamuzi ya pamoja badala ya kiomgozi kutoa amri kwa walio chini yake ama kuwatenga kimamlaka.
Hata hivyo Kardinali de Aviz amesema ameridhishwa kushiriki mkutano huo wa Watawa (ACWECA).
Amesema amaguswa na liturujia ya Misa Takatifu hapa Tanzania ambayo ilimfanya asali mara mbili kwani niliturujia hai yenye utamadunisho ndani yake.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU