“SITASAHAU UTAJIRI WA LITURUJIA TANZANIA” KARDINALI JOAO

n Na Pascal Mwanache, Dar

RAis wa Baraza la Kipapa la Maisha ya waliowekwa wakfu Mwadhama Joao Kardinali Braz de Aviz amewaasa waamini nchini kudumisha utamadunisho katika maadhimisho ya Misa Takatifu huku akishangazwa na utajiri mkubwa wa liturujia nchini Tanzania.
Amesema hayo alipoongoza adhimisho la Misa Takatifu ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 17 wa Shirikisho la Masista Wakatoliki nchi za Afrika Mashariki na Kati (ACWECA), uliofanyika katika Kanisa la Bikira Maria Mkingiwa dhambi ya asili, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Kurasini jijini Dar es salaam.
“Nimestaajabishwa na namna ambavyo neno la Mungu limeletwa hapa mbele, ukitanguliwa na moto katika chungu kuonyesha mwanga wa neno la Mungu, huo ni wito kwa watawa kuliishi neno hilo kwa furaha katika utume wenu. Taswira hii itabakia katika maisha yangu. Kwa kweli tamaduni zenu zina nguvu mno” ameelezea Kardinali Joao.
Ameongeza kuwa amefurahishwa na Liturujia nchini Tanzania ambayo inaakisi urithi wa utamaduni na kukiri kuwa liturujia hiyo ni tofauti sana na ile anayoishuhudia akiwa Vatikani.
“Nimefurahishwa na urithi wa utamaduni katika Liturujia yenu, hii ni tofauti sana na kile nachokiona kule Vatikani. Utamaduni wenu na karama viende sambamba, kamwe msiviache” amesisitiza.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU