"MSIANDIKE MABAYA YA AFRIKA TU"




Waandishi wa habari waafrika wametakiwa kutoa kipaumbele kwa habari za bara la Afrika.
Katika hotuba iliyosomwa na mratibu wa mawasiliano wa AMECEA Padri Chrisantus Ndaga kwa niaba ya Mwenyekiti wa Catholic News Agency For Africa (CANAA)Askofu Mkuu Charles Palmer Buckle wa Jimbo kuu Accra Ghana katika mafunzo ya uandishi wa habari za mtandaoni unaofanyika jijini Nairobi,imeonekana kuwa baadhi ya vyombo vya habari vinajikita zaidi katika mabaya ya bara la Afrika wakati yapo mambo mengi na mazuri yanayofanywa na kanisa barani humo hayaandikwi wala kutangazwa.
Mambo yanayopewa kipaumbele ni pamoja na migogoro,rushwa,magonjwa pamoja na mambo mengine yanayolipa sifa mbaya bara hilo.
Padri Ndaga ameonyesha matumaini kwa waandishi wakatoliki waliotoka katika nchi za Kenya, Uganda, Tanzania, Zambia, Zimbabwe, Shelisheli, Malawi, Nigeria, Ghana na Sudani Kusini kuwa watayatumia mafunzo hayo kubadili uandishi unaolififisha bara la Afrika.
Mafunzo hayo ya siku nne yameandaliwa na CANAA.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU