“Bila uwajibikaji na uwazi Kanisa litakosa miradi”

MAKATIBU wa Idara ya Uchungaji na Mawasiliano wameaswa kuwa mawakala sahihi wa utawala wa rasilimali, uwajibikaji na uwazi katika utekelezaji wa miradi inayofadhiliwa na wafadhili ili kusaidia shughuli mbalimbali Kanisa.
Hayo yamesisitizwa na Naibu Katibu Mkuu wa AMECEA, Padri Chrisantus Ndaga wakati wa warsha juu uratibu madhubuti wa rasilimali fedha na watu  kwa  Makatibu wa Idara ya Uchungaji na Mawasiliano pamoja na baadhi ya wanachama kutoka Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Afrika Mashariki (CUEA) na baadhi ya wahabari watendaji kutoka nchi wanachama wa  AMECEA
Padri Ndaga amewasisitiza  washiriki kuwa makini na ubunifu ili kusaidia ofisi zao na mabaraza yao kwa lengo la kuwa na maendeleo  endelevu.
“Lengo la warsha hii  ni kutoa ujuzi kwa Waratibu wa kichungaji, Mawasiliano na wanahabari wetu ambao wanahusika moja kwa moja katika kuendeleza ofisi za mawasiliano na Kichungaji ili wapate elimu juu ya uhamasishaji wa rasilimali fedha na kuanzisha uhusiano mzuri na washirika ili kutoa huduma bora kwa Kanisa.
Katika mahojiano maalum, na mwezeshaji wa semina Hillary Korir, ambaye ni Mkurugenzi wa Caritas Jimbo Katoliki Nakuru Kenya amesema semina ni wakati muafaka kwa sababu umeleta pamoja waratibu wa Uchungaji na Mawasiliano ambao kwa kweli wanahitaji elimu ya utawala na kumudu  rasilimali ili kuboresha ujuzi wao na kupata maarifa juu ya kuandika miradi na ripoti zinazokidhi vigezo vya wafadhili na Kanisa kwa ujumla.
"Hapo awali ilikuwa ni rahisi kupata fedha za wafadhili kuendesha shughuli za Kanisa. Ungeweza kuandika karatasi moja ukapata fedha. Lakini leo hii unapaswa kuandikamambo mengi kwakutii vigezo vya wafadhili kwani wanaoomba msaada ni wengi kuliko wanaotoa. Siku hizi mambo yamebadilika mahitaji ni ya watu wengi, ushindani ni mkubwa na si rahisi kupata fedha tena, "amesema.
Katika mada yake, mwezeshaji alibainisha kuwa miradi mingi hukataliwa na na wafadhili kutokana na sababu kadhaa ikiwa ni pamoja na kuandika matatizo yasiyoeleweka, miradi isiyo na vigezo katika  mahitaji fulani, kushindwa kuandika ripoti kwa wakati, , ukosefu wa uwajibikaji na kukosa ujuzi wa kuandaa miradi.
“Zamani waliokuwa wanaandikamiradi walikuwa ni wataalamu wa miradi lakini dunia imebadilika kila mmoja katika ofisi yake iwe ni ya uandishi wa habari, elimu, liturujia, afya nk. Kila mtu anapaswa kuwa na utaalamu wa kuandika mradi ili kukidhi mahitaji ya Kanisa na ofisi husika. Hivyo wanamawasiliano hii ni fursa ya kuleta maendeleo chanya katika kujitegemeza na kuinjilisha kwa kina. Kinachotakiwa ni kuwa wabunifu wa miradi,” amesisitiza.
Washiriki walikuwa changamoto kwa kujifunza na kuwa na sanaa ya kuendeleza mapendekezo, kuhusisha washauri ikiwa ni lazima, kuendeleza mapendekezo kwamba kushughulikia mahitaji maalum ya jamii na wakati huo huo, kujitahidi kuunganisha mipango kwa manufaa ya jamii.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mawasiliano Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya Bw. David Omoyo amesisitiza kuwa katika kila ofisi ya Baraza la Maaskofu lazima kila mmoja achangamkie fursa za kuandika miradi wakati anaangalia zipi changamoto, fursa, udhaifu na vitisho vya miradi anayoiandika.
“Unaweza kuandika mradi yako ukauona ni bunifu wenye utaalamu wa hali ya juu kumbe kuna wengine zaidi ya 3000 wameandika miradi kama yako kwa kuwa matatizo ya Kanisa wakati mwingine ni yaleyale. Hivyo ukiwa mbabaishaji katika kuandika hususani matokeo ya mradi mzima pia changamoto hutapata na wala hawatasoma. Hivyo ujuzi wa hali ya juu unatakiwa,” amesisitiza.
Ameshauri kila mmoja katika ofisi za mabaraza ya Maaskofu Katoliki nchi za AMECEA kuwa na ubunifu wa kutaka kujiendeleza kwa kuandika miradi mbalimbali badala ya kutegemea mtu maalumu wa kuandika mradi.

“Mtu maalumu anaweza kuwepo lakini mara nyingi anachelewesha mambo kwani anakuwa na shughuli mbalimbali. Ni vyema kila mmoja akajifunza ili kurahisisha kazi na kuleta ufanisi zaidi.”

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU