KONGAMANO LA EKARISTI TAKATIFU 2020 KUFANYIKA JIMBO KUU TABORA



MAaskofu, mapadri na waamini wa majimbo Katoliki Kanda Ya Magharibi wameanza maandalizi rasmi ya kuwa wenyeji wa Kongamano la Ekaristi Takatifu kitaifa mwaka 2020.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao cha siku moja cha maandalizi hayo Jimboni Tabora, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Tabora Mhashamu Paulo Ruzoka amewaomba wana Kanda ya Magharibi kumshukuru Mungu kwa kupewa heshima kubwa na Kanisa la Tanzania kwa kuwa wenyeji wa Kongamano hilo kitaifa hivyo ni vema washirikiane katika kufanikisha kazi hiyo ya Mungu.
Baadhi ya mambo yaliyojadiliwa katika kikao hicho ni pamoja na majimbo yanayounda Kanda hiyo ya Magharibi kukusudia kuandika kitabu kitakachotoa historia nzima ya Ukristo ndani ya majimbo hayo. Pamoja na historia hiyo pia historia ya Ukristo toka mlango wa Imani Bagamoyo nayo pia itaandikwa.
Akizungumza na Gazeti hili Askofu Mkuu Ruzoka amesema majimbo yote yanaandaa utaratibu wa kupata wawezeshaji wa Mada mbalimbali zitakazotolewa juu ya Ekaristi Takatifu ili kuongeza uelewa kwa washiriki watakaoshiriki katika kongamano hilo.
Inakadiriwa washiriki wa kongamano hilo watakuwa 6,700 na gharama ya kila mshiriki itatolewa baada ya gharama halisi kuwa imebainishwa na kamati ya inayoratibu gharama za kila mshiriki na kutumwa hapo baadaye ili kila mtu anayependa kushiriki aanze maandalizi mapema.
Maaskofu walioshiriki mkutano huo ni:  Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Tabora Mhashamu Paulo Ruzoka, Askofu wa Jimbo Katoliki Kahama Mhashamu Ludovick Minde na Askofu wa Jimbo Katoliki Kigoma Mhashamu Joseph Mlola.
Kongamano hilo linatarajiwa kuzinduliwa rasmi tarehe 30 Juni 2020 Jimboni Tabora.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU