MADAKTARI WATANZANIA WAENDELEA KUCHANGAMKIA FURSA ZA AJIRA 500 KENYA

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto Ummy Mwalimu amewashauri madaktari wa Tanzania ambao hawana ajira za serikali na wanakidhi vigezo waendelee kuomba nafasi za ajira nchini Kenya, huku akitaja idadi ya waliokwishaomba.
Kutpitia mtandao wake wa twitter, Waziri Ummy amesema hadi sasa ndani ya siku moja pekee, tayari kuna madaktari zaidi ya 150 tayari wamekwishaomba nafasi hizo.

"Sisi tunaendelea kupokea Maombi. So far, kwa siku ya 1 tu tumeshapokea zaidi ya 150! Naendelea kutoa Wito kwa MDs wetu kutoiacha fursa hii." Ameandika Waziri Ummy Mwalimu.
Amesema mwisho wa kutuma maombi hayo ni tarehe 27 Machi, 2017.

Serikali ya Tanzania hivi karibuni ilikubali kuwapeleka madktari wake 500 nchini Kenya, kutokana na mgogoro unaoendelea nchini humo, uamuzi ambao umepingwa na vyama vya madaktari vya nchi zote mbili yaani Tanzania na Kenya.

Kwa mujibu wa taarifa aliyoitoa Waziri huyo, alisema kwa sasa Tanzania haina tatizo la madaktari, bali kuna changamoto ya kuwaajiri madaktari waliopo.

"Katika kipindi cha mwaka 2013/14 hadi 2016/17 madaktari 2,439 wamehitimu. Kati ya hao serikali imeajiri 615 tu. Pia watakaoajiriwa mwaka 2017/18 hawatazidi 600 ..... Hivi sasa hatuna tatizo la uwepo wa madaktari. Changamoto yetu ni kuwaajiri tunaozalisha" Alisema Ummy

Alisema Tanzania kwa sasa ina uwezo kuzalisha takribani madaktari 1,200 kwa mwaka."

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU