Kanisa lajitosa kunusuru uharibifu wa mazingira Mlima Wotta

VIONGOZI  wa  Kanisa  Katoliki  Parokia    ya  Kibakwe,  Jimbo  Kuu  Katoliki  Dodoma,  wamesema  kuwa   endapo   serikali  haitazuia  uharibifu wa  mazingira  katika  Milima  ya  Wotta  ambayo  ndiyo  chanzo  cha  maji kwa  vijiji  takribani 10 vya  wilaya  hiyo,  wilaya hiyo huenda ikakumbwa na  uhaba  mkubwa  wa  maji na ukame.
Viongozi   hao wakiongozwa  na  Padri  Selestine  Lipambile na  viongozi  wengine   waliotoka  vigango  vya  Lukole  na  Kingiti   wametembelea milima hiyo ili kuangalia  uwezekano  wa  Kanisa  kusaidia  upatikanaji  wa  maji  ya  uhakika  toka  vyanzo  vya  maji  ya  vijiji  hivyo.
Katika tathmini yao wamebain kuwa uharibifu  wa  mazingira  katika  vyanzo  hivyo  ndiyo chanzo kikuu cha uhaba wa maji ulioanza kukumba wakazi wa maeneo hayo kitu  ambacho  serikali  wilayani  humo  wameshindwa  kuzuia .
Wakitoa  mfano  wa uharibifu  mkubwa  ulifanyika  katika  mlima  wa  viongozi hao wamejionea eneo  hilo  likiwa limeharibiwa  kwa  kugeuzwa   eneo   la   mashamba   huku   kukiwa   na  chanzo  hicho  kikuu  cha  maji  cha  vijiji  hivyo . Wamesema  kuwa  ni  jambo  la  ajabu  serikali  imekaa  kimya  wakati  watu  wanaendelea  kuteseka   kwa   kukosa  maji  ya  uhakika.
Akiongelea   tatizo  hilo  Padri Lipambile  amesema kuwa   kutokana  na  shughuli za kilimo kufanyika katika vyanzo vya maji, hali hiyo imesababisha mchanga  kujaa  katika  chanzo  hicho  kwa  sababu  hakuna  miti  na  kuwafanya  wananchi  wa  kata  nzima  ya  Kingiti  kukosa  maji  kwa miaka mingi.
Padri  Lipambile   ameongeza  kuwa   viongozi  wa  eneo  hilo  wameliomba    kanisa  kuangalia   uwezekano   wa  kusaidia  upatikanaji  wa  maji  eneo hilo  lakini  kutokana na kukithiri kwa shughuli za  kilimo  cha  ovyo  katika  chanzo  hicho  na  vyanzo  vingine  kanisa   halioni  haja  ya  kusaidia  kwani  msaada  huo  utakuwa  kazi  bure  kama  kilimo  na  uharibifu  huo  utaendelea  bila  serikali  kuchukua  hatua  kali  dhidi   ya  waharibifu  hao .
“Ulegevu wa viongozi wetu hapa ndiyo  uliotufikisha  hapa  tulipo,  kwa  sababu  ya  kulinda maslahi ya  mtoto   wa  mjomba  au  mtoto  wa  shangazi” amesema .
           


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU