Dada wadogo wa Yesu wameacha utume Afghanstan

BAADA ya miaka 60 ya huduma kwa wahitaji , Shirika la Dada wadogo wa Yesu   limelazimika kuacha kutoa huduma katika  mji wa Kabul Afghanstan   na kulazimika kufunga nyumba zao kutokana na ukosefu wa miito.
Hayo yameelezwa na Padri Giuseppe Moretti ambaye amefanya utume kwa muda wa miaka 18 mji Mkuu  Kabul kama msimamizi wa Kanisa lao dogo.
Padri huyo amekuwa kwa muda mrefu na hakuacha mji mkuu wakati wa kuingiliwa na  jeshi la Kisovietiki na hata kwa wanajeshi wa kitaleban au wakati wa mabomu ya hapa na pale.
Akitoa ushuhuda juu ya historia ya watawa hawa anasema; kuwa kipigo na mateso ya namna hii yamewafanya watawa hawa kuishi na watu karibu, hata walipofika wanajeshi wa Nato mwaka 2000 kutaka kuwahoji watawa hawa hawakupendelea kutoa habari zozote kuhusu watu wao walio kuwa wakiishi nao.
Hiyo siyo kwa sababu ya kuogopa ya kwamba wataonekana kama wapelelezi bali ndiyo ilikuwa mtindo na karama yao ya kuhudumia watu kwa ukimya katika mateso.
Watu wengi walifika kwa watawa  kuomba msaada,waliwasikiliza kwa upendo historia zao na zilibaki ndani ya mioyo yao.
Ili kuweza kushirikiana na wakazi hao,watawa hawa waliweza kuongea lugha ya wenyeji ili kushiriki bege kwa bega na watu rahisi na masikini , kwa njia hiyo watawa walipendwa na kusifiwa na jumuiya nzima ya watu kiasi kwamba miaka ya hivi karibuni  walikuwa wametunikiwa uraia wa Afghanstan.
Watawa wa Dada wadogo wa Yesu waliheshimiwa sana hata na maaskali wa Waktalebani.
Anakumbuka kwamba mwaka 1993 wakati wa vita,  Ijumaa wote walikuwa wanakwenda hata katika kikanisa cha Ubalozi kusali, japokuwa Kikanisa hicho kilikuwa imefungwa kwa sababu ya vita vya wenyewe kwa wenyewe. Watalebani waliwatambua ni wakina nani na hivyo waliaacha waingie kusali.
Mbele ya Kikanisa hicho kuna msalaba mkubwa unaoonekana.  Nyumba ya watawa hao ilikuwa karibu na sehemu ya ubalozi, kwa njia hiyo wangeweza hata kuharibu Kanisa hilo lakini hawakufanya hivyo. Ijapokuwa mtawa wa mwisho kuondoka ilikuwa ni mwezi Februari 2017, historia yao ni muhimu kabisa katika nchi hii ya Afghanistan, Padri Moretti anaongeza.
Hawa ni watawa walioitikia wito kujibu upendo wa  Mungu  na kumfuasa Kristo katika kuiishi Injili .
Ni roho iliyojikita katika ukimya  wa kujitoa, sala , urafiki na matendo kwa kukumbatia ulimwengu.
Shirika hili lilianzishwa na Mgdaleine wa Yesu kwa ushirikiano na Mwenyeheri Charles de Foucauld maarufu kama Padri wa kiroho aliyeishi katika maeneo ya jangwa.
Mwenyeheri Charles de F. anakumbukwa sana na wosia mwingi wa kiroho katika maisha ya waamini kila siku kwani ni kutokana na uzoefu wake kabla ya kumtambua Mungu ni nani kwake, nawakati anajitafakari maisha yake aliandika maneno kwa kumwelekea Mungu akisema “Kama upo ee Mungu nipe neema ya kukutambua” lakini  baada ya kumjua ya kwamba  Mungu yupo akasema  “Asingeweza kufanya lolota zaidi ya kuwa naye mpaka milele” (1901). Kwa njia hiyo watawa wa kike na kiume wamefuata nyayo zao za Yesu wa Nazareth kwa kutoa  huduma yao pande zote za dunia.
Upendo wa Yesu Mwenyeheri Charles de F. ulisababisha yeye kuwa ndugu wa wote bila ubaguzi na ameandika kwamba “utume wangu unapaswa uwe wa wema. Kwasababu atakaye niona lazima asema kwakuwa mtu huyu ni mwema na hivyo dini yake lazima ni nzuri.”
Vilevile anasema  “Kama nikiulizwa kwani mimi ni mpole na mwema, lazima kusema kwasababu mimi ni mtumishi wa mtu aliye mzuri zaidi ya mimi”.
 Anaongeza , ”Kama tungelijua jinsi gani Bwana Yesu ni mwema,… ninatamani niwe mwema zaidi hadi wasema , kama mtumishi huyo ni mwema hivyo , Je Bwana wake yuko je?”.
Mwanzilishi Mkuu wa Shirika Charles de Foucauld akiwa na Mgdaleine wa Yesu ameandika tafakari nyingi sana za kiroho kuonesha upendo mkubwa wa Yesu alio kuwa nao ambazo ni urithi kwa waamini wengi , pamoja na kwamba ndiyo mwongozo wa dada wadogo wa Yesu ambao kwa miaka 60 wameweza kufanya huduma ya kitumea katika nchi ya Afghanstan na sasa wameng’atuka kwasababu ya kukosefu wa miito katika eneo hilo.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU