TUTUMIE KWARESIMA KUSAIDIA WAHITAJI- KAMANDA WA JESHI LA POLISI RUKWA








Kamanda wa jeshi la Polisi mkoa wa Rukwa Kamishna Msaidizi wa polisi George Simba Kyando amewataka watanzania kutumia vema kipindi hiki cha Kwaresima kwa kuachana na dhambi na badala yake kuwasaidia wahitaji mbalimbali katika jamii.

Akikabidhi msaada wa bidhaa mbalimbali kwa watoto yatima katika kituo cha malezi cha mt. Martin de porres kilichopo katandala kinachomilikiwa na shirika la masista wa Maria Mtakatifu Malkia wa Afrika MMMMMA Jimboni sumbawanga  kwa niaba ya jeshi la polisi mkoani Rukwa kamanda kyando amesema kuwa ni vema jamii ikatambua uhitaji wa vituo vya watoto yatima kwa kusaidia huduma na mahitaji kwa watoto pasipo kujali nafasi za kazi,vyeo,madaraka,hali za maisha dini au siasa kwani wlelewa si wa dini wala kabila
Hatua hii imekuja ambapo jeshi la polisi mkoani rukwa linaadhimisha wiki ya kipolisi mkoa na kwa kipindi hiki cha kwaresima limeona ni vema kutoa mchango kwa watoto yatima.
Akipokea mchamgo huo kutoka jeshi la polisi mama mkuu mlezi wa kituo hicho Sister Scholastika Wampembe amelishukuru jeshi la polisi mkoa wa Rukwa kwa kujali na kuguswa na maisha ya watoto yatima na kutoa wito kwa jamii wananchi,serikali, mashirika ya dini na makampuni binafsi kuendelea kusaidia kwani ni changamoto nyingi zinazowakabili katika malezi ya watoto hao ambapo kwa sasa kina jumla ya watoto 31.

Kituo cha Mt. Martin de pores kilianzishwa mwaka 1963 katika parokia ya mwazye na baadae kuhamishiwa manispaa ya Sumbawanga mnamo mwaka 1974 kwaajili ya kuboresha huduma zake ambapo kinapokea watoto kutoka sehemu mbalimbali ndani ya nchi bila kujali dini,rangi,kabila na Taifa.

Kituo hiki kilianzishwa kwa malengo ya kuwatunza watoto wanaofiwa na mama zao baada ya kuzaliwa, kutunza watoto wanaotelekezwa na mama zao wakiwa wachanga na watoto ambao wazazi wao wana ulemavu wa akili.

Kituo cha kulelea watoto yatima cha martn de pores kinakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo ukosefu wa mishahara ya wafanyakazi, huduma za umeme,maji,dawa na huduma zingine za kimalezi kwa watoto yatima

Na Emmanuel Mayunga, Rukwa

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU