SALA YA ASUBUHI. Kwajina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina. Ee Baba yetu Mungu mkuu, Umenilinda usiku huu. Nakushukuru kwa moyo, Ee Baba, Mwana na Roho. Nilinde tena siku hii, Niache dhambi, nikutii. Naomba sana Baba wee, Baraka zako nipokee. Bikira safi, Ee Maria Nisipotee nisimamie. Mlinzi mkuu malaika wee, Kwa Mungu wetu niombee Nitake nitende mema tu, Na mwisho nije kwako juu. Amina. NIA NJEMA. Kumheshimu Mungu wangu Namtolea roho yangu, Nifanye kazi nipumzike Amri zake tu nishike Wazo, neno, tendo lote Namtolea Mungu pote Roho, mwili chote changu, Pendo na uzima wangu Mungu wangu nitampenda, Wala dhambi sitatenda. Jina lako nasifia, Utakalo hutimia. Kwa utii navumilia Teso na matata pia. Nipe, Bwana, neema zako Niongeze sifa yako. Amina. SALA YA MATOLEO. Ee Yesu, kwa mikono ya Bikira Maria, na kwa maungano na sadaka yako kuu, ninakutolea sala, matendo, masumbuko na furaha zangu zote za leo. Ee Yesu, ufalme wako utufikie. BABA YETU. Baba yetu uliye mbinguni, jina ...
Na Charles Rwehumbiza UINJILISHAJI BAGAMOYO NA TANZANIA KWA UJUMLA Kutokea Bagamoyo, wamisionari wa Shirika la Roho Mtakatifu waliweza kuendelea kuinjilisha sehemu mbalimbali za Tanzania kama vile Mhonda (Morogoro), Mandera (Morogoro), Kilema Kibosho (Moshi) na Kondoa, n.k. Kutokana na ugumu wa watu wa Bagamoyo kukubali Injili na uamuzi wa wamisionari wenye asili ya Uholanzi kuhamia Morogoro mjini. Bagamoyo iliachwa kwa kipindi kirefu bila huduma za mapadri au wakiwa wanapata huduma ya Misa Takatifu mara moja kwa mwezi. Jambo hili lilisababisha ukuaji wa Kanisa la Bagamoyo kuwa duni sana hadi mwaka 1992 padri mwafrika wa kwanza alipoingia na kuweka makazi ya kudumu Bagamoyo. Padri huyu wa kwanza mwafrika kuinjilisha Bagamoyo sio mwingine ila Padrei Valentine Bayo wa Shirika la Roho Mtakatifu. Tangu aingie Bagamoyo, Padri Bayo chini ya usimamizi wa shirika lake, ameweza kuipa Bagamoyo hadhi iliyo nayo leo hii. Hakika haitakuwa vibaya kumwita Padri Bayo ...
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya mabadiliko madogo katika safu ya wakuu wa mikoa na amewateua wakuu wa wilaya 139. Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika mabadiliko hayo Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi. Zainab R. Telack kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga. Bi. Zainab R. Telack anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Anna Kilango Malecela ambaye uteuzi wake ulitenguliwa. Rais Magufuli pia amemteua Dkt. Binilith Satano Mahenge kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma. Dkt. Binilith Satano Mahenge anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabit Mwambungu ambaye amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu Dar es salaam ambako atapangiwa majukumu mengine. Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. Charles F. Mlingwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara. Dkt. Charles F. Mlingwa anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Stansla...
Comments
Post a Comment