SALA YA ASUBUHI. Kwajina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina. Ee Baba yetu Mungu mkuu, Umenilinda usiku huu. Nakushukuru kwa moyo, Ee Baba, Mwana na Roho. Nilinde tena siku hii, Niache dhambi, nikutii. Naomba sana Baba wee, Baraka zako nipokee. Bikira safi, Ee Maria Nisipotee nisimamie. Mlinzi mkuu malaika wee, Kwa Mungu wetu niombee Nitake nitende mema tu, Na mwisho nije kwako juu. Amina. NIA NJEMA. Kumheshimu Mungu wangu Namtolea roho yangu, Nifanye kazi nipumzike Amri zake tu nishike Wazo, neno, tendo lote Namtolea Mungu pote Roho, mwili chote changu, Pendo na uzima wangu Mungu wangu nitampenda, Wala dhambi sitatenda. Jina lako nasifia, Utakalo hutimia. Kwa utii navumilia Teso na matata pia. Nipe, Bwana, neema zako Niongeze sifa yako. Amina. SALA YA MATOLEO. Ee Yesu, kwa mikono ya Bikira Maria, na kwa maungano na sadaka yako kuu, ninakutolea sala, matendo, masumbuko na furaha zangu zote za leo. Ee Yesu, ufalme wako utufikie. BABA YETU. Baba yetu uliye mbinguni, jina ...
Na Charles Rwehumbiza UINJILISHAJI BAGAMOYO NA TANZANIA KWA UJUMLA Kutokea Bagamoyo, wamisionari wa Shirika la Roho Mtakatifu waliweza kuendelea kuinjilisha sehemu mbalimbali za Tanzania kama vile Mhonda (Morogoro), Mandera (Morogoro), Kilema Kibosho (Moshi) na Kondoa, n.k. Kutokana na ugumu wa watu wa Bagamoyo kukubali Injili na uamuzi wa wamisionari wenye asili ya Uholanzi kuhamia Morogoro mjini. Bagamoyo iliachwa kwa kipindi kirefu bila huduma za mapadri au wakiwa wanapata huduma ya Misa Takatifu mara moja kwa mwezi. Jambo hili lilisababisha ukuaji wa Kanisa la Bagamoyo kuwa duni sana hadi mwaka 1992 padri mwafrika wa kwanza alipoingia na kuweka makazi ya kudumu Bagamoyo. Padri huyu wa kwanza mwafrika kuinjilisha Bagamoyo sio mwingine ila Padrei Valentine Bayo wa Shirika la Roho Mtakatifu. Tangu aingie Bagamoyo, Padri Bayo chini ya usimamizi wa shirika lake, ameweza kuipa Bagamoyo hadhi iliyo nayo leo hii. Hakika haitakuwa vibaya kumwita Padri Bayo ...
KATIKA kutolea maoni kibwagizo changu cha jana cha “WOTE KIMYAA!!”, mwenzetu Deonatus F. N. Mutani ametaka kutuchanganya sote. Mimi nawatafuta “wachawi” au “watu wenye uchawi” wanyeshe mvua siku hizi tupone. Nataka wajitokeze tuone. Nataka wajitokeze hadharani watende kitu cha kutufaa sote. Nimekataa uwapo wa uchawi na wachawi kati yetu. Tulionao ni wababaishaji na watu tunaowatuhumu kwa kuwasengenyasengenya tu. Wachawi kiukweli hawapo na bado ninawatafuta. Ninataka wajitokeze na nimesema kama kuna anayewajua awataje, atuitie au atuoneshe wenzake. Mwenzetu Deonatus Mutani ametoka huko niliko na kusema eti Biblia inakiri kuwapo kwa uchawi na wachawi. Ndipo amenishangaa mimi ni padre wa aina gani kukataa uwepo wa uchawi ambao kwa kadiri yake unashuhudiwa na Biblia yake. Sawa. Lakini leo hii tukimuuliza mwenzetu huyu Biblia gani hiyo, bila shaka atasema ni Biblia ya Kiswahili au ya Kiingereza fulani. Kumbe, hapo ndipo atakapokosea na ndipo panaponipa mimi fursa ya kutoa somo la ...
Comments
Post a Comment