Maaskofu Kanisa Katoliki Kanda ya Magharibi wapiga kambi jimboni Sumbawanga.





Maaskofu wa Kanisa Katoliki Kanda ya Magharibi wamepiga kambi ya siku tano jimboni Sumbawanga kwa ajili ya kujadili mipango ya kichungaji na maendeleo ya utume katika kanisa Katoliki Kanda ya Magharibi .
Wakiongoza na mwenyeji wao Mhashamu Askofu Damian Kyaruzi wa Jimbo Katoliki la Sumbawanga, wengine ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Tabora Mhashamu Askofu Paul Ruzoka na Askofu Gervasi Nyaisonga wa Jimbo Katoliki Mpanda. Wengine ni Askofu Joseph Mlola wa Jimbo Katoliki Kigoma na Askofu Rudovik Minde wa Jimbo Katoliki Kahama ambayo inajumuisha majimbo matano likiwemo Jimbo Kuu Tabora.
Akiwapokea maaskofu hao, mwenyeji wao Askofu wa Jimbo Katoliki Sumbawanga Mhashamu Damian Kyaruzi amesema kuwa maaskofu hao wanakutana metropolitan ya Tabora ambapo waliazimia kuwa kila mwaka kwa pamoja watakua wakizungukia majimbo yote kwa lengo la kufanya mikutano yao na kufanya shughuli za kichungaji katika majimbo na maazimio hayo yanaanzia katika Jimbo Sumbawanga kuanzia tarehe 25 May hadi tarehe 29 Mei mwaka huu.
 Wakiwa jimboni sumbawanga maaskofu hao wanatarajia kuwa na mkutano wa maaskofu wa kanda katika kumbi za uaskofuni pamoja na kutoa kipaimara katika parokia za Kristo mfalme, parokia ya kanisa kuu, parokia ya Familia Takatifu na katika seminari ndogo ya kaengesa
Akitoa Baraka kwa waamini wa Jimbo Sumbawanga mara  baada ya mapokezi Askofu Mkuu wa Kanda ya Magharibi Mhashamu Paul Ruzoka amewashukuru waamini wa Jimbo Sumbawanga kwa mapokezi na kuwaomba wadumu katika sala na  daima na kusimama imara katika imani ya Kristo mfufuka hasa kwa kipindi hiki cha kuhitimisha kipindi cha Pasaka.

 Na Emanuel Mayunga Sumbawanga





Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU