‘Padri asiyependa waamini hakubaliki’ Ask Nzigilwa

n Na Pascal Mwanache

IMEELEZWA kuwa kitendo cha waamini kuwapenda mapadri wao ni matokeo ya namna ambavyo mapadri wanajitoa kwa upendo katika kuwahudumia waamini hao. Hayo yamesemwa na Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es salaam Mhashamu Eusebius Nzigilwa katika Misa Takatifu ya kutoa Daraja Takatifu ya Upadri kwa shemasi Dominic Mavula wa Shirika la Damu Azizi kutoka Parokia ya Mandela Jimbo Katoliki Morogoro.
Askofu Nzigilwa amesema kuwa padri anapaswa kutoa huduma yake huku akitambua kuwa kupenda na kuwa na huruma ni nyenzo muhimu katika kuhusiana na kuhudumia waamini. Amesema kuwa utume wa padri ni kuokoa roho za waamini na siyo roho yake pekee.
“Sala, moyo wa huruma na upendo ni sehemu ya utume wa padri. Mkiwapenda waamini nao watawapenda kwa kuwa upendo ni lugha inayoeleweka na viumbe vyote. Hivyo mjitahidi kuishi huruma na upendo wa kimungu, na kwa kufanya hivyo mtazipeleka roho nyingi mbinguni” ameeleza.
Aidha Askofu Nzigilwa ameongeza kuwa huruma ya padri kwa waamini ni lazima iendane na roho na bidii ya kusali, kwa kuzingatia imani na usikivu katika sauti ya Mungu. Hata hivyo Askofu Nzigilwa amewaasa waamini kuwapokea mapadri na kuwasaidia katika mapungufu yao na kuwatia nguvu.
“Muwapokee mapadri na muwasaidie, mfanye kazi yao iwe sababu ya wokovu kwao na kwenu. Wao wameteuliwa kwa ajili ya utakatifu na kuokoa roho za waamini siyo kuokoa roho zao pekee. Hivyo muwasaidie katika mapungufu yao na kuwatia nguvu” ameongeza.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU