USHEMASI IRINGA



ASKOFU wa Jimbo Katoliki Iringa Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa amezindua mwaka wa Jubilei ya miaka 100 ya mapadri wazalendo na kuwataka waamini kuendelea kuwaombea mapadri popote walipo.
Uzinduzi wa jubilei hiyo umefanyika kwenye kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu Parokia ya Kihesa kwa  kuwashwa kwa mshumaa mara baada ya Askofu Ngalalekumtwa kumaliza kutoa daraja la ushemasi kwa mafrateli Jerome Mtatifikolo wa parokia ya Ilole na Jerome Mponzi wa parokia ya Nyakipambo.
Akitoa homilia kwenye misa hiyo Mhashamu Ngalalekumtwa amesema kwamba, sambamba na utoaji wa daraja hilo lakini pia waamini wanatakiwa kuwaombea viongozi wa Serikali ili waweze kutenda kazi zao kiuaminifu.








Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU