“Shirikishaneni kumaliza maradhi ya kiroho” Askofu Mkude



MOROGORO, “Moyo mlionao wa kushikana mikono na kutatua yanayowakabili mwilini kama magonjwa na kadhalika muwe na ushirikiano huo huo kutatua maradhi ya rohoni yanayowakabili.”
Rai hiyo imetolewa hivi karibuni na Askofu  wa Jimbo Katoliki Morogoro  Mhashamu Telesphor Mkude alipokuwa akihubiri kwenye maadhimisho ya hija ya Wanawake Wakatoliki Tanzania(WAWATA) iliyoazimishwa katika parokia ya Mgeta.
Askofu Mkude amesema binadamu wamekuwa wepesi kusaidiana kwenye mambo ya mwilini kama magonjwa, sherehe na mengineyo yahusuyo mwili lakini ushirikiano huo haupo kwenye kutatua magonjwa ya kiroho.
“Kuna watu wanaumwa na magonjwa ya rohoni hivyo mtu anapokuja na kukueleza jambo lake msikilize kwa makini wengine misaada wanayotaka siyo ya fedha, chakula wala mavazi ila wanataka wasaidiwe kiroho na amani yao ipatikane,” amesema Askofu Mkude.
Amesema mtu ambaye shida yake ni ya kiroho ni lazima itatuliwe kiroho na usikatishwe tamaa katika shida aliyonayo kwa kuwa umeshindwa kuitatua wewe mpeleke ngazi za juu ili asaidiwe kutatua.
“Unaposhindwa kutatua shida ya mtu ya kiroho usimkatishe tamaa kwa kumwambia hii haiwezekani, badala yake mpeleke ngazi za juu ili asaidiwe inawezekana wewe msaada wako ndio umeishia hapo lakini shida yake ikikutana na mtu wa masuala ya kiroho  inatatulika,” amesema Askofu Mkude.
Pia amesisitiza wale ambao wapo na shida za kiroho wasikubali kukatishwa tamaa wanapotafuta utatuzi wa shida zao na badala yake waende ngazi kwa ngazi bila kuchoka mpaka wapate ufumbuzi ili wawe na amani mioyoni mwao.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU