SAUT yafanya Mahafali ya 18

CHUO Kikuu cha Mtakatifu Augustino Mwanza (SAUT) ambacho kinamilikiwa na  Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania kinafanya mahafali yake ya 18 tangu kuanzishwa kwake.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari uliohudhuriwa na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari nchini, Makamu Mkuu wa Chuo hicho Padri Dkt, Thaddeus Mkamwa amesema sherehe hizo za mahafali zinafanyika kwa siku mbili yaani Desemba 16 na 17 mwaka huu.
Amebainisha kuwa takribani wahitimu 3000 wa vitivo  mbalimbali wanahitimu kwa nyanja tofauti na kuwa wamegawanya mahafali hayo kwa siku mbili kwa ajili ya wingi wa wanafunzi na kurahisisha shughuli hiyo.
Mgeni rasmi ni  Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki  Mwanza Mhashamu Thaddeus Ruwaichi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Vyuo Vikuu Katoliki Tanzania ambaye anamwakilisha Mkuu wa Chuo hicho yaani (Chancellor) Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa ambaye ni Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania na pia Askofu wa Jimbo la Iringa.
Katika mkutano huo Padri Dokta Mkamwa ameongeza kua mahafali hayo yametanguliwa na siku ya maonesho ya chuo ambayo yanajulikana kama (SAUT community day) yaliyofanyika Novemba 14 katika uwanja wa chuo hicho ali maarufu kwa jina la Raila Odinga ambapo wanafunzi pamoja na wahadhiri wao watashiriki katika maonesho hayo mbalimbali kutoka katika kila kitivo na idara huku wakijumuika na jamii inayowazunguka.
“ SAUT inajivunia mafanikio yake kuanzia kuanzishwa kwake mnamo mwaka 1998 ikijulikana kama Nyegezi (Social Training) kabla hakijabadilishwa kuitwa SAUT,ambapo kilianza na wahitimu 102 na mpaka sasa takribani kimeweza kuhitimisha takribani wanafunzi 30,000 tangu kuanzishwa kwake.
Chuo kimejitahidi kuweka elimu sawa kwa wanafunzi wote wa kike na wakiume na pia kua kimekua na mahusiano mazuri na mataifa mbalimbali kutoka nchi za nje,na kua kwa mwaka huu wa masomo 2016/2017 SAUT kimeweza kupokea wanafunzi kutoka  mataifa mbalimbali yakiwemo China, Ujerumani, Finland, Marekanina Canada ambapo wanafunzi hao wanakuja kujifunza chini ya makubariano kati ya SAUT na vyuo vyao (Bilateral agreements),” ameeleza Padri Mkamwa.
Aidha ameeleza kuwa, chuo hicho pia kinafundisha masomo ya lugha za nje ikiwemo kifaransa na kichina kwa walimu, wanafunzi na wafanyakazi. Hivyo amewasihi watu wengi wajitokeze kusoma kichina ili waweze kukabiliana na soko la ajira kwa kuzingatia China sasa ni taifa lenye guvu kiuchumi duniani.
Ameongeza kua katika mafanikio hayo pia chuo kinajivunia kutoa wanafunzi imara na shupavu na pia wenye nidhamu watakao enda kulitumikia taifa kwa Nyanja zote, na kua wanafunzi wote kutoka katika program mbalimbali wameshiriki mafunzo yako katika mafunzo ya vitendo kwa taasisi na mashirika mbalimbali.
Vilevile amesema kuwa mwaka huu chuo hicho kina wahitimu watatu wa shahada ya uzamili (PhD) wakitokea katika kitivo cha sayansi ya mahusiano ya umma yaani PhD in mass communication.
Aidha amebainisha kua takribani wanafunzi 746 hawataweza kuhitimu katika mahafari hayo kwa sababu zao binafsi ikiwemo  kukosa sifa za kuhitimu yaani kutofanya vizuri katika masomo yao, wengine kuahirisha mwaka na pia kushindwa kufanya mtihani yao kwa sababu ya kiuchumi.
Aidha amebainisha changamoto mbalimbali zinazokikumba chuo hicho ukiwemo uhitaji wa vifaa vya kufundishia mfano vifaa tiba na uhandisi, ukosefu wa wachangiaji yaani wanafunzi na serikali pale wanapochelewa kutoa ada kwa wakati na pia asilimia chache ya wanafunzi ambao wanakua hawapo tayari kusoma na kusababisha idadi ya wanafunzi wanaoshindwa kuhitimu kuongezeka.
Hivyo kutokana na changamoto hizo inalazimu chuo kutafuta pesa za ziada kuendelea kufundisha na kutoa wanafunzi walio bora.
Katika mahafali hayo ya 18 tangu kuanzishwa kwake yamebebwa na ujumbe ‘Changia katika mchango wa SAUT katika kuandaa nakutoa wahitimu bora na mahili kwa jamii.’

SAUT ni chuo kikuu cha katoliki ambacho tangu kuanzishwa kwake kimeweza kuzaa takribani vyuo vitatu ambavyo mpaka sasa vinajitegemea  yaani MWECAU, RUCU na CUHAS Bugando

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU