MUSOMA WAPATA VIONGOZI HALMASHAURI YA WALEI

Picha ya pamoja  wajumbe wa Halmashauri ya Walei Jimbo katoliki Musoma walioshiriki  uchaguzi wa kuwapata viongozi wapya, uchaguzi uliosimamiwa na  Mwenyekiti wa Halmashauri  kutoka Taifa Ndugu Gasper Mathew Makululi na Alvera Kabwogi ambaye ni mtunza hazina wa Halmashauri ya Walei Taifa uliofanyika katika ukumbi wa Conference Centre Jimbo la Musoma hivi karibuni(picha na Veronica Modest)



Picha ya pamoja  viongozi wapya wa Halmashauri ya Walei Jimbo katoliki Musoma waliochaguliwa wakiwa na  Mwenyekiti wa Halmashauri  kutoka Taifa Ndugu Gasper Mathew Makululi na Alvera Kabwogi ambaye ni mtunza hazina wa Halmashauri ya Walei Taifa uliofanyika katika ukumbi wa Conference Centre Jimbo katoliki Musoma hivi karibuni(picha na Veronica Modest)

Naibu Askofu wa Jimbo katoliki Musoma na msimamizi wa uchaguzi Padri Julius Ogolla (katikati) akiwatizama Mwenyekiti wa Halmashauri  kutoka Taifa Ndugu Gasper Mathew Makululi  kutoka jimbo katoliki Moshi (kushoto) na Alvera Kabwogi ambaye ni mtunza hazina wa Halmashauri ya Walei Taifa kutoka Jimbo kuu katoliki Dar Es Salaam(kulia) wakihesabu karatasi za kura katika uchaguzi wa kuwapata viongozi uliofanyika katika ukumbi wa Conference Centre Jimbo la Musoma, hivi karibuni(picha na Veronica Modest)



 Picha ya pamoja Naibu Askofu wa Jimbo katoliki Musoma  Padri Julius Ogolla, Mwenyekiti wa Halmashauri  kutoka Taifa Ndugu Gasper Mathew Makululi  kutoka jimbo katoliki Moshi  na Alvera Kabwogi ambaye ni mtunza hazina wa Halmashauri ya Walei Taifa kutoka Jimbo kuu katoliki Dar Es Salaam baada ya kumaliza uchaguzi uliofanyika katika ukumbi wa Conference Centre Jimbo la Musoma,Hivi karibuni(picha na Veronica Modest)
 

Veronica Modest ,Musoma.
 
Halmashauri ya Walei Jimbo katoliki Musoma  imepata viongozi wapya ambao wataongoza kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia 2016 hadi 2019 , katika mkutano wa  uchaguzi huo uliofanyika Oktoba 1, mwaka huu katika ukumbi wa Conference centre uliopo Jimboni Musoma .
 
Kabla ya uchaguzi  huo, wajumbe wa mkutano huo wakiongozwa  na viongozi kutoka Halmashauri ya Walei Taifa, walianza kwa semina ya siku moja wakijifunza juu ya umuhimu wa kutenga fungu la kumi, semina  iliyoongozwa na  Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo kutoka Taifa Ndugu Gasper Mathew Makululi  kwa kushirikiana na Alvera Kabwogi ambaye ni mtunza hazina wa Halmashauri ya Walei Taifa.
 
Baada ya semina hiyo yalifuata mafungo kwa ajili ya kumuomba Mwenyezi Mungu aweze kuwasaidia wapate viongozi bora watakaolitumikia kanisa na Jimbo  kwa uaminifu, na uchaguzi huo ulisimamiwa na viongozi wa Kitaifa pamoja na Naibu Askofu wa Jimbo la Musoma Padri  Julius Ogolla na kubahatika kuwapata viongozi  watakaowaongoza katika kipindi hicho.
 
Viongozi waliochaguliwa ni  Raymond Nyamasagi -Mwenyekiti kutoka parokia ya Mugumu, Alex Malima Kisurura -Makamu Mwenyekiti kutoka Parokia ya Musoma Mjini, Richard Getenyi - Katibu kutoka Parokia ya Nyamiongo, Julius Magige  - Katibu Msaidizi kutoka Parokia ya Tarime na Joseph Getunguye – Mweka hazina Kutoka  parokia ya  Mugumu
 
Akizungumza mara baada ya uchaguzi, Mwenyekiti Mpya wa Halmashauri hiyo Raymond Nyamasagi aliwashukuru sana wajumbe hao kwa kumpatia viongozi ambao watashirikiana katika kufikia malengo ya Halmashauri hiyo, sambamba na kuwahamasisha wajumbe wote walioshiriki kuhakikisha kile walichojifunza wanakwenda kuwafunza waamini wao ili kuonyesha muungano mzuri ndani ya Kanisa.
 
Kwa upande wake katibu ambaye ndiye msimamizi mkuu wa shughuli za halmashauri hiyo ndugu Richard Getenyi aliwaomba wajumbe  kupitia parokia zao kuhakikisha wanajitahidi kushiriki kikamilifu, ili kuweza kusaidia katika kutekeleza shughuli mbalimbali za kila siku pamoja na kulipa michango  mbalimbali mapema kwa ajili ya mkutano mkuu wa kitaifa.
 
Baada ya uchaguzi huo viongozi hao wakiongozana na wajumbe wa mkutano huo walishiriki ibada ya kuwabariki viongozi hao ,ambayo iliongozwa na Paroko wa Makutano Padri Julius Ogolla.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU