‘Kipaumbele cha Padri ni Ekaristi Takatifu’

PAROKO wa Parokia ya Isimani Padri Leornad Maliva amewaasa mapadri kuangalia vipaumbele vya utume wao hasa wanapopangiwa maeneo mapya ya kazi.

Padri Maliva ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Mapdri Jimbo Katoliki  Iringa (UMWAI) amesema, suala la msingi kwa padri yeyote anapopangiwa eneo jipya la uchungaji ni uwepo wa Ekaristi Takatifu na sio umeme, barabara ya lami na mitandao ya simu. Padri ahakikishe kuwa katika ratiba yake ya kila siku anapanga muda wa kukaa na Yesu wa Ekaristi Takatifu.

“Padri hana sababu yeyote inayomfanya akose muda wa kuabudu Ekaristi kila siku. Padre ni mwadhimishaji wa Ekaristi Takatifu na ni vema aiabudu hata baada ya misa.

Katika sakramenti ya Ekaristi Takatifu, Yesu ametuachia ukumbusho wa mateso yake ili mateso na mahangaiko yetu yapate faraja katika kuiabudu hiyo Ekaristi.
Kwa padri, kuabudu Ekaristi takatifu ni kielelezo cha unyenyekevu wa kukubali kuwa padre ni kiumbe dhaifu anayepata na kuchota nguvu za utume wake katika ukumbusho wa mateso ya Yesu kwenye sakramenti ya ajabu, yaani Ekaristi takatifu.
Padri Maliva ameyasema hayo katika sherehe ya Jubilei ya miaka 25 kwa Padri Charles Muna, Br. Damian Wissa ambaye ametiza miaka 25 ya utawa na Sista Maria Kasela (CST) aliyefunga nadhiri za kwanza, sherehe ambazo zimefanyika katika Kanisa la Bikira Maria Imakulata parokia ya Kaning’ombe Jimbo Katoliki Iringa.

Ninafahamu mawasiliano katika ulimwengu wa sasa ni jambo la msingi na muhimu lakini si kipaumbele kwa padri kwani kipaumbele cha Padri  ni Injili na Ekaristi Takatifu. Network ni baada ya Injili na Ekaristi.

Inapendeza kuwasiliana na wengine na kupata habari kama haki msingi ya mwanadamu lakini Padri asikatae, ama kusononeka kupelekwa kwenye eneo la kazi ambako kuna changamoto za mtandao.
Suala la kwanza ni uwepo wa waamini, Kanisa, Ekaristi Takatifu, Injili na mahitaji msingi ya mwanadamu kama malazi na chakula ili aweze kuhudumia watu wa Mungu.

Tunaadhimisha miaka 100 ya Upadri na miaka 150 ya Ukristo Tanzania Bara. Zipo changamoto mbalimbali a wamisionari wa Kwanza amabo hawakuwa na mitandao, simu, magari na walikuta watu hawamju Kristo wakaanza kuhubiri bila kukata tamaa hadi tumefika hapa tulipo leo.

Hivyo nasi katika changamoto zetu za utandawazi, usitutoe nje ya utume wetu ukatufanya watumwa badala ya kuwa watumwa wa Injili. “Ole wangu nisipoihubiri Injili.” Amesisitiza Padri Maliva.

Amesema kwamba haipendezi kwa mtumishi wa Mungu kujali mambo ya dunia ambayo ki msingi hayana kipaumbele kwao.

“Wenzetu wanatukumbusha kushukuru Mungu kwa wito tuliopewa kama zawadi kutoka kwake.  Ni vyema tukawa na moyo wa shukrani na kufurahia utume wetu,” amesisitiza Fr Maliva.

Awali Paroko waparokia hiyo Padri Charles Mwipopo amesema kwamba wanamshukuru Mungu kwa kufikia sherehe hizo kwani mara mbili wameihirisha kutoka na afya ya Padri Muna kutokuwa nzuri.

Misa hiyo iliongozwa na Pelate  Monsinyori Julian Kangalawe  na homilia imetolewa na Padri Maliva.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU