Askofu Minde azidua Jubilei ya miaka 100 ya Upadri Kahama

ASKOFU LUDOVICK Minde wa jimbo la Kahama amezindua rasmi Jubilee ya miaka 100  ya padri na kutoa wito kwa  mapadri kuupenda na kuuenzi  upadri wao ambao ni zawadi kutoka kwa Mungu.

Akihubiri  katika Misa Takatifu ya uzinduzi wa Jubilei hiyo iliyofanyika  hivi karibuni katika Kanisa Kuu la jimbo la Mtakatifu Karoli Lwanga Parokia ya Kahama mjini Askofu Minde amewasisitiza mapadri  kuutunza upadri kama lulu  uweze  kuonekana  katika utume wao kwa Kanisa.

Aidha amewakubusha mapadri wajibu wao na kuwataka  kuendelea kuomba neema  hiyo  ya kuupenda  zaidi upadri , kuuenzi  kwa sababu ni zawadi  kuu ya  milele toka  kwa  Mungu  aliyowajalia  ndani ya kanisa kwa kushirikishwa ukuhani huo.

“Mapadri wanahitaji kuombewa katika utume wao ili waweze kung’aa  kama mwanga  katika  dunia hii  katika  utumishi wao  wa uijilishaji  kwa kumunganisha mtu na mafumbo  ya  mbinguni wanapoazimisha misa .

Mapadri wameshirikishwa ukuhani huo kwa mfano wa Melkisedeki Kuhani Mkuu na kutoa wito kwa  waami  kuwaombea kwa sala, kuwatunza, kuwasaidia, kuwapenda na kuwapa ushirikiano  waweze kutimiza wajibu wao  katika  kumtumikia  Mungu kwenye maisha  yao,” amesisitiza.


Amesema kuwa, katika dunia ya sasa yenye utandawazi mapadri na watawa  wanakumbwa na  changamoto mbalimbali hivyo ni rahisi kutoka nje ya maisha yao na kufwata ya kidunia, hivyo   amewataka waamini walei kuwasaidia mapadri na watawa kuishi wito wao, waache kuwapotosha katika mambo mbalimbali ya ulimwengu.

Wakati huohuo katika Jimbo la Kahama , Askofu Minde ameadhimisha Misa Takatifu ya kuweka Nadhili za Kwanza za Utawa kwa Masista watatu wa shirika la Mabinti Masikini wa Bikira Maria iliyofanyika katika Parokia ya Jina Takatifu la Yesu, Bukombe.

Askofu Minde amewataka wazazi na walezi  katika familia  kuwaruhusu  watoto wanapokuwa na wito wa kumtumikia Mungu na kuwasaidia kufikia wito huo.

“ Ndugu zangu wazazi waruhusuni watoto kujiunga na maisha ya utawa pale Mungu anapowaita. Msiwachagulie miito kwani wito unatoka kwa Mungu pekee,” amesisitiza Askofu Minde.


Aidha askofu Minde katika kazi zake za kichungaji alitoa sakramenti ya kipaimara kwa watoto 581  wa Parokia ya Mtakatifu Stephano Shahidi na kusisitiza umuhimu wa mafundisho ya Kanisa  Katoliki kwa watoto ili wawe wafuasi imara wa  imani  kwa Yesu Kristo.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU