Kimbiji wasali kwenye banda la miti
WANAJUMUIYA ya Mtakatifu Yohane Mbatizaji
Kijaka Parokia ya Kimbiji jijini Dar es salaam wametakiwa kutokata tamaa
kutokana na mazingira magumu ya kuabudu.
Rai hiyo imetolewa na Padri Thomas Laurent
baada ya kuwatembelea wana jumuiya hao siku ya Dominika na kushuhudia mahali
wanapoabudia ambapo ni banda la miti
lililopo katikati ya pori lililo wazi na kuezekwa kwa minyaa.
Wakizungumza na gazeti la Kiongozi
wanajumuiya hao wamesema ni kwa mda mrefu sasa wanasali katika kibanda hicho na
hali hiyo inatokana na umbali mrefu uliopo kati yao na Parokia. Wamesema
inawachukua takribani saa saba kutembea mpaka Parokiani jambo lililowapa ugumu
na wakaamua kujenga banda hilo ambapo Padri hufika eneo hilo kwa gari kwa ajili
ya Misa ya Ibada Takatifu.
Aidha Padri Thomas amezitaka Parokia na watu binafsi ndani ya Kanisa
kuwasaidia wanajumuiya hao ili wapate mazingira mazuri ya kuabudia na pia
amewataka waamini hao kujikwamua kwa hali na mali ili wapate kujenga angalau Kanisa
dogo la matofali kwa kushirikiana na wadau (waamini) kutoka parokia nyingine.
Comments
Post a Comment