Kimbiji wasali kwenye banda la miti



WANAJUMUIYA ya Mtakatifu Yohane Mbatizaji Kijaka Parokia ya Kimbiji jijini Dar es salaam wametakiwa kutokata tamaa kutokana na mazingira magumu ya kuabudu.
  Rai hiyo imetolewa na Padri Thomas Laurent baada ya kuwatembelea wana jumuiya hao siku ya Dominika na kushuhudia mahali wanapoabudia ambapo ni banda la miti  lililopo katikati ya pori lililo wazi na kuezekwa kwa minyaa.
     Wakizungumza na gazeti la Kiongozi wanajumuiya hao wamesema ni kwa mda mrefu sasa wanasali katika kibanda hicho na hali hiyo inatokana na umbali mrefu uliopo kati yao na Parokia. Wamesema inawachukua takribani saa saba kutembea mpaka Parokiani jambo lililowapa ugumu na wakaamua kujenga banda hilo ambapo Padri hufika eneo hilo kwa gari kwa ajili ya Misa ya Ibada Takatifu.
  Naye mwenyekiti wa jumuiya hiyo Bi .Paulina Jeremia ameliambia gazeti la Kiongozi kuwa, wazo la kujenga banda hilo la kuabudia limeokoa waamini wa Jumuiya hiyo waliokuwa kwenye hatari ya kubadili imani yao kutokana na umbali na ugumu wa kushiriki katika ibada. Jumuiya hiyo yenye waamini zaidi ya 25 bado haijatambulika kuwa Kigango japokuwa ina kila kitu cha kutambuliwa kama Kigango.

       Aidha Padri Thomas amezitaka  Parokia na watu binafsi ndani ya Kanisa kuwasaidia wanajumuiya hao ili wapate mazingira mazuri ya kuabudia na pia amewataka waamini hao kujikwamua kwa hali na mali ili wapate kujenga angalau Kanisa dogo la matofali kwa kushirikiana na wadau (waamini) kutoka parokia nyingine.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU