WANAWAKE KUONGOZA NAFASI ZA JUU KANISANI?

Papa Francis ameongoza majadiliano ya kina hapo jana juu ya jukumu la wanawake kanisani akisema 
anaangalia uwezekano wa kuanzisha tume ya kuchunguza uwezekano wa kurejesha
mashemasi wa kike.Mazungumzo yake ilikuwa ni sehemu ya swali katika kikao cha
pamoja na baadhi ya viongozi 900 wa umoja wa wanawake wa kanisa ambao ni sehemu
ya Umoja wa Kimataifa uitwao UISG.Hata hivyo jambo hilo la kihistoria
haliwaruhusu wanawake kuongoza misa bali watasimamia ubatizo,sala na mambo
mengine.Haya yatakuwa mageuzi makubwa katika KARNE nyingi zilizopita huku
katika karne ya 1 wanawake waliwahi kupewa nafasi hizo ila wakaacha. 
 

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU