"TEC WAFUNDWA"



WAFANYAKAZI wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) wamepatiwa semina ya siku moja iliyolenga kuwajengea uwezo wa kufahamu na kuendana na mpango mkakati wa TEC katika utendaji wao.

Katika semina hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano TEC, wafanyakazi hao wameelezwa juu ya umuhimu wa kuzingatia tunu msingi za Baraza hilo la maaskofu, ili utendaji wao wa kazi uendane na mabadiliko yaliyomo katika mpango mkakati huo.

Akizungumza na wafanyakazi hao ndugu Stephen Shayo ambaye ni mwezeshaji katika semina hiyo ameeleza kuwa kuundwa kwa mpango kazi huo ni matokeo ya tathmini iliyofanywa na Maaskofu ili kuendana na mahitaji ya utendaji kazi ya sasa.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Padri Raymond Saba amewahimiza wafanyakazi wa TEC kudumu katika kufanya kazi kwa bidii bila woga ili kuendana na mabadiliko hayo.

























Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU