WAONYESHENI NJIA SAHIHI WAAMINI-ASKOFU MINDE






Askofu Minde amesema hayo katika mahubiri kwenye misa ya kuhitimisha mkutano  mkuu wa  wajumbe  wa  chama cha kitume cha Shirika la Moyo Mtakatifu wa Yesu waliokutana jimboni katoliki Kahama.



Askofu Minde  amesema baadhi ya waamini wamekuwa wakikosa mwelekeo katika maisha yao na kuomba vyama vya kitume kuwasaidia  katika mambo ya imani ya kanisa katoliki na kuwarudisha katika mwelekeo mzuri kuanzia ngazi ya familia na  jumuiya ndogondogo.



Aidha amesema  uwepo wa shirika la Moyo Mtakatifu wa Yesu ndani ya  kanisa  kwa sala  na maombezi linapaswa kupongezwa huku akilihimiza kutunza    usafi wa  moyo  katika  mambo ya  uijilishaji, kuendelea zaidi na ibada zao  na kulitangaza shirika ili waamini  wa rika zote  waweze  kujiunga nalo.



Viongozi wa Shirika la Moyo Mtakatifu wa Yesu  toka majimbo yote katoliki nchini ambao ni wajumbe wa  mkutano  mkuu  wa Taifa    wamekuwa na  kikao  chao  cha  siku  tano jimboni  Kahama  ambapo pamoja  na kujadili maendeleo ya  utume wao pia wamefanya uchaguzi wa viongozi wa  kitaifa .



Viongozi wa kitaifa waliochaguliwa katika mkutano mkuu  wa  shirika la Moyo Mtakatifu wa Yesu  ni Mwenyekiti  Longinus Kagaruki , makamu mwenyekiti  Christopher  Mrope , Katibu mkuu ni  Richard Mahundi , Katibu Msaidizi Ernesta Mosha , Muweka Hazina  Martina Kisaka na muweka hazina msaidizi ni Fredrick Leonard.





Na  Patrick Mabula , Kahama .


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU