TAASISI ZA KIDINI KUWENI MACHO NA ARDHI MNAYOMILIKI-WAZIRI AONYA

Stan Likomawagi na Rodrick Minja, Dodoma

BARAZA la Maaskofu Tanzania (TEC), Mtandao wa Tume ya Haki na Amani Afrika (AFJN),Wamissionari wa Damu Takatifu ya Yesu na baadhi ya taasisi za Kiraia  wameandaa Kongamano juu ya haki katika uporaji wa ardhi, madhara kwa aatanzania na Afrika.

Kongamano hilo la siku mbili  limefanyika  Septemba 14-15 mwaka huu mjini Dodoma katika Hoteli ya Mtakatifu Gaspar likiwashirikisha wanamazingira, wasomi, watunga sera, wakulima,Viongozi wa Dini, wawakilishi wa taasisi za kiraia na wadau wengine.

Katika kufungua Kongamano hilo, Naibu waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angelina Mabula amezitahadharisha taasisi za kidini hapa nchini kuhakikisha zinakuwa na hati ya umiliki wa maeneo ya ardhi waliyoyanunua kwaajili ya shughuli mbalimbali za maendeleo.


Amesema kuwa, Serikali inatambua juhudi kubwa zinazofanywa na mashirika au taasisi za kidini katika kuleta maendeleo hasa kwa kujenga shule, zahanati, hospitali na miradi mingine.

 Hivyo zinahitaji ardhi ya kutosha lakini ili ziepuke migogoro na matatizo ya uporaji wa ardhi lazima zihakikishe zinakuwa na hati miliki za maeneo waliyonunua.

Dkt Mabula amesema kuwa, tatizo la uporaji wa ardhi Barani Afrika ni kubwa mno na linatishia amani na ustawi wa bara hili, hata hivyo kumekuwa na namna tofauti za kulitazama tatizo hilo.

Amefafanua kuwa wakati mwingine kumekuwa na mkanganyiko miongoni mwa wadau juu ya nini hasa maana ya uporaji wa ardhi hivyo aliwataka washiriki wa kongamano hilo katika mijadala yao waje na uelewa wa pamoja wa dhana hii ili iwe rahisi kushughulikia tatizo hilo.

“Wakati mwingine matukio ya uporaji wa ardhi yamekuzwa kupita kiasi na vyombo vya habari ,wanaharakati au wanasiasa ambao wana malengo ya kushinda chaguzi hali ambayo hukimbiza wawekezaji wazuri ambao wanahitaji kukuza uchumi na kuboresha maisha ya watanzania” amesema waziri Mabula.

Hata hivyo alisisitiza kuwa ardhi ni rasilimali ambayo ni lazima impatie manufaa mmiliki. Ardhi isiyotumika vizuri kiuzalishaji haina maana.

Amesema kuwa, serikali imekuwa ikiboresha mazingira bora ya uwekezaji katika ardhi ili wananchi wa kawaida na wawekezaji wakubwa wapate kipato kutokana na Ardhi yao. Ametaja juhudi hizo za Serikali ni pamoja na kupanga, kupima na kumilikisha ardhi kwa kutoa hati za kawaida na hati za kimila.

Waziri Mabula amesema kuwa, katika kuhakikisha taratibu na sheria zinafuatwa katika umiliki wa ardhi kwa sasa serikali imeanza kutwaa ardhi kwa watu waliohodhi maeneo makubwa hasa vijijini bila ya kuyaendeleza katika baadhi ya mikoa ikiwemo Tanga na mengineyo na pia itatwaa viwanja visivyoendelezwa.

“Utakuta katika baadhi ya maeneo hasa vijiji kuna watu wamehodhi mashamba makubwa ambayo yamegeuka mapori bila ya kuyaendeleza hali hii inasababisha chuki baina ya wamiliki na wananchi ambao hawana ardhi kwa ajili ya shughuli mbalimbali ikiwemo kilimo na ufugaji kitendo kinachosababisha kuvamia eneo hilo na kujigawiya,” amesema waziri huyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtandao wa Haki na Amani Afrika Padri Aniedi Okure amesema kuwa, tatizo la uporaji wa ardhi katika bara la Afrika ni kubwa kwani asilimia 50.

Amesema hali hii inatokana na kukithiri kwa vitendo vya Rushwa ambayo imekuwa ni saratani katika kukuza maendeleo kwa nchi za Afrika pamoja na ukosefu wa uadilifu na utawala bora baadhi ya viongozi.
Padri Okule ameongeza kwamba, wananchi wamekuwa wakihadaiwa kupitia kivuli cha uwekezaji kwamba wakitoa ardhi watapata maendeleo lakini baadaye hawanufaiki na jambo lolote kutoka kwa wawekezaji hali inayosababisha chuki na migogoro isiyokwisha.



Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU