ASKOFU KYARUZI AHIMIZA MSAADA KWA WAHANGA WA TETEMEKO

Na Emanuel Mayunga Sumbawanga

ASKOFU kwa Jimbo Katoliki la Sumbawanga Mhashamu Damian Kyaruzi amewataka wakristo na watu wote nchini kuwasaidia waanchi wa mkoa wa Kagera katika maafa waliyopata hivi karibuni kutoakana na tetemeko la Ardhi lililosababisha vifo kadhaa, kuharibu majengo na mali.

Askofu Kyaruzi ameyasema hayo wakati akifungua kongamano la siku 8 la hija ya Mwaka wa Huruma ya Mungu lililoanza  Septemba 11 katika viwaja vya Libori Center Manispaa ya Sumbawanga  na kuhitimishwa jumapili ya 18 Septemba mwaka huu katika mlima wa hija maarufu kwa jina la Itwelele uliopo manispaa ya Sumbawanga.

Katika kongamano hilo askofu Kyaruzi amesema kuwa katika nyakati hizi watu hawajali wala kuguswa na matatizo ya wengine hasa wanaokubwa na maafa na ajali zinazosababisha vifo, majeruhi na hata wengine kukosa makazi./ Baadhi wanaona kama si sehemu ya maisha yao kwakuwa hayatokei sehemu walipo

‘Ndugu zangu wakristo na watanzania wote tunapaswa tutambue kwamba, kuwa na huruma hakuhitaji dini, huruma si ya kabila, huruma si ya taifa, sura, rangi, tajiri au masikini bali ni hisia na mguso wa ndani ambao mtu anaona thamani ya mwenzake katika mahitaji aliyonayo na kumsaidia kutatua au kuondoa kile ambacho kinamfanya mwingine akose amani.

Tuwajali wenzetu bila kujali tofauti zetu. Kwenye maafa pasiwepo siasa, ukabila wala matabaka. Huruma ni kielelezo cha upendo’.

Aidha askofu kyaruzi  mwaka wa Huruma ya Mungu unasisitiza kuomba huruma na kuhurumia wengine. Ndio maana dunia ya sasa ina vita kila mahali lakini chanzo chake ni kukosa upendo, unyenyekevu na msamaha kwa wengine.

“Dunia yetu vita vimetawala baina ya taifa na taifa watu kudhulumiwa kwa ajili ya imani yao,  watu wanapoteza makazi kwa ajili ya imani yao na tumeshuhudia wakimbizi katika kila kona ya dunia hii na hasa afrika yetu. Mauaji ya watoto na utoaji mamba na kila aina ya unyanyasaji mbalimbali.

Haya ni matokeo ya kutokuwa na huruma kwa wengine. Na sisi sote kwa kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine tumekuwa wazito wa kutowakimbilia wenye shida na kutokuwasaidia na haya yote yanatokana na kutojali na kuguswa na matatizo ya wengine na kuona ni ya watu.

Mfano hivi karibuni tumesikia maafa yaliyotokea kule Kagera ya tetemeko la ardhi ambalo na sehemu tofauti mabweni ya wanafunzi kuungua moto, mafuriko na mambo kadha wa kadha yanayolikumba taifa  lakini  watu hatujali wala kuguswa kana kwamba hayatuhusu.
Huko ni kukosa moyo wa huruma na upendo.

Kwa kusoma alama za nyakati Ndio maana Baba mtakatifu April 11, 2015 aliitisha mwaka wa Yubilee ya Huruma ya Mungu ili kuhamasisha kupendana, kushikamana, kujaliana na kusaidiana na hivyo huruma iongoze maisha yetu na tuweze kuguswa na kusaidia wahitaji katika taifa letu,” amesema Askofu Kyaruzi.

Kwa zaidi ya miaka 20 jimboni Sumbawanga kumekuwa kukifanyika kongamano kubwa la mahubiri ya hadhara maarufu kwa jina la poplamission ambalo hubeba ujumbe wa Mwaka wa Kanisa uliotangazwa na Baba Mtakatifu ambalo tamasha hili hufanyika kila mwezi wa tisa kuelekea dominika ya kutukuka kwa msalaba na kuhudhuriwa na maelfu ya wakristo na wasio wakristo.

Kongamano hilo huhitimishwa katika vilele vya mlima wa Itwelele  (milanzi) mlima ambao ni maarufu sana kwa historia ya  kabila la wafipa ambapo inasadikika ndipo chimbuko la kabila hili kupitia kwa viongozi wake wa jadi (watemi) ambapo juu ya kilele chake kuna msalaba wa hija ambapo watu mbalimbali hufika kusali na kufanya hija na novena zao .

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU