UZINDUZI WA GROTO NA KAMUSI YA LITRUJIA YA KANISA KATOLIKI ULIVYOFANA KATIKA PICHA 15 JIMBONI DAR ES SALAAM

Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam limefanya uzinduzi wa GROTTO(kanisa dogo) mpya ya Bikira Maria pamoja na KAMUSI YA LITRUJIA KATOLIKI, matukio ambayo yamefanyika kwenye Sikukuu ya Mtakatifu Yosefu kwa adhimisho la Misa Takatifu iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu jimboni humo.

Uzinduzi huo umefanywa na Mwadhama Polycap Kardinali Pengo, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Dar es Salaam akishirikiana na Askofu Msaidizi wa Jimbo hilo Mhashamu Eusebius Nzigilwa pamoja na Mapadri kadhaa na waamini kwa ujumla.

Kamusi hiyo itatumika kutoa tafsiri halisi ya maneno kama yanavyotumika katika kanisa katoliki huku grotto ikitumika kwa ajili ya waamini kumpelekea Mwenyezi Mungu maombi yao kupitia kwa Mama Bikira Maria.(Pichani Askofu Mkuu wa Jimbo kuu la Dar es salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo akizindua kamusi ya Litrujia)

Adeline Berachimance 

Zifuatazo ni baadhi ya picha za uzinduzi huo..


















Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU