"MAPADRI MSIKATISHWE TAMAA" ASKOFU PAULO RUZOKA


MHASHAMU Baba Askofu Mkuu Paulo Ruzoka wa Jimbo kuu Tabora amewaomba mapadri wote nchini kutoa huduma zao kwa waamini bila kuchoka wala kukata tamaa na daima wao waseme sisi ni watumishi tusio na faida tumefanya tuliyopaswa kufanya.

Askofu Ruzoka ametoa rai hiyo wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu aliyoiadhimisha katika kanisa la kuu la jimbo la Mtakatifu Theresia wa mtoto Yesu Tabora.

Akihubiri,Askofu amesema mapadri hawana budi kudumu kwa uaminifu hasa juu ya ahadi walizoweka wakati walipopewa Sakramenti ya upadrisho.

Aidha katika ibada hiyo ya Misa Takatifu mafuta ya wagonjwa,wakatukumeni na Krisma takatifu yalibarikiwa.

“Mafuta haya tunayoyabariki ni zana za kazi hivyo mapadre wayatumie katika kuhudumia waaamini,wapange vizuri ratiba zao za utume ili waweze kuwatembelea wagonjwa kusikiliza matatizo yao na kuwapa huduma ya sakramenti ili kuwapa matumaini na uhakika wa safari yao yakumrudia Muumba wao”.

Kuhusu mwaka wa Huruma ya Mungu ameshauri kila muumini anapaswa kutumia mwaka huu  kuona na kuonja Huruma ya Mungu kwa wanadamu na kuwa tayari kuipeleka huruma hiyo kwa wengine akibainisha kuwa huu ni mwaka wa kupatana na kufanya toba ya kweli.
 
Askofu Ruzoka pia amesema majuma sita ya kwaresima ni kipindi ambacho waamini wanapaswa kutafakari kwa kina kuhusu ufuasi wao kwa Kristu;
Aidha amesema wanadamu wanapaswa kuwa na moyo wa shukrani katika mafaniko yoyote kwani Mungu ndiye mweza wa yote.

“Tuwe tayari kumuomba radhi Mwenyezi Mungu pale tulipofanikiwa na kudhani tumeweza yote kwa uwezo wetu na ubunifu wetu”.

Askofu Ruzoka amesema mwanadamu anapokutana na changamoto asikate tamaa bali ajue hayuko peke yake bali yupo na Kristu na kusanyiko kama hili ni vema liwe la kutiana moyo katika utume na kusaidiana bila kuhubiria wengine wakati wao wakiangamia.

Askofu Ruzoka amewatia moyo mapadri kutokata tamaa pale wanapotafsiriwa tofauti na walivyo bali watambue kuwa hata Kristu hakupendwa na wote,ndiyo maana akateswa na kufa msalabani.

Ibada hiyo ya Misa imehudhuriwa na mapadri,watawa,waseminaristi wakubwa(Kipalapala seminari)na waamini wa parokia ya Mtakatifu Theresia wa Mtoto Yesu na parokia za jirani.





Na pd MamboT 



 Baadhi ya waamini wakishiriki Ibada ya Misa takatifu katika kanisa la kiaskofu Tabora.Na pd Mambo T.

 Mhashamu Baba Askofu Mkuu Paulo Ruzoka muda mfupi kabla ya kuanza maandamano. Na pd Mambo T

 Mhashamu Baba Askofu Ruzoka akichanganya manukato  katika mafuta ya Krisma takatifu. Na pd.Mambo T.

Mhashamu Baba Askofu Ruzoka akipokea mafuta matakatifu.

Wanakwaya wa kwaya ya Watakatifu mashahidi wa Uganda , Tabora

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU