"FUNGUENI MILANGO KWA WAKIMBIZI"PAPA AWAAMBIA VIONGOZI DUNIANI


Baba mtakatifu Papa Francis amewataka viongozi duniani kuwaruhusu kuingia nchi mwao wakimbizi na wahamiaji wanaokimbia kwao kutokana na vita na migogoro.
Amesema si vizuri kuwazuia kuingia nchini watu ambao wamekimbia kwa mwendo mrefu bila kula wala kunywa,wakiwa na hofu,maumivu na kumbukumbu za wapendwa wao waliowapoteza.
Watu hawa waweza kujiuliza Mungu yupo wapi?inawezekanaje mateso makali hivi kuwapata watu wasiokuwa na hatia,watoto na wanawake?amesema Papa.
Papa amesema ni faraja kuwaona viongozi wengi na serikali zao wakifungua mioyo yao na kuwaruhusu wakimbizi na wahamiaji kuingia nchini mwao pasipo kikwazo chochote.
Papa Francis ameyasema haya akizungumza na karibu mahujaji 40,000 waliokuwa wakimsikiliza katika eneo la Mtakatifu Petro.
Katika katekesi yake juu ya huruma kwa njia ya maandiko,amelenga katika sura ya 30-31 katika kitabu cha Yeremia ambacho pia hujulikana kama kitabu cha faraja kutokana na matumaini ambayo nabii huyo aliyatoa kwa wafuasi wake.
Papa Francis amewaonyesha wasikilizaji wake jinsi gani nabii Yeremia alikwenda kwa wana wa Israeli waliokuwa uhamishoni na akawatangazia kurudi katika nchi yao.
Papa Francis ameeleza kuwa sisi pia tuna uzoefu wa aina ya kifungo kuwa kuna wakati uzoefu wa mateso na kifo hutufanya sisi kufikiri kwamba Mungu ametuacha.
Papa amehitimisha kwa kuomba Mwenyezi Mungu awabariki wote wanaoishi katika hali kama hizo na kuwalinda kutokana na maovu.
CNA/EWTN News 

Comments

  1. Vizuri Baba Mtakatifu Francis Kwan unaonyesha mfano mzuri kwa waamini wako na watu wote kwa ujumla, Mungu akuzidishie neema na baraka zake.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU