PAPA FRANCIS RASMI INSTAGRAM:APATA WAFUASI ZAIDI YA MILIONI MOJA SIKU YA KWANZA







BABA Mtakatifu Fransisko amezindua akaunti mpya ya picha kwenye mtandao wa Instagram, mtandao wenye mvuto mkubwa kwa vijana wa kizazi kipya.

Baada ya kujiunga na Instagram Machi 19, 2016 Papa tayari amepata watu milioni 1.5 wanaomfuatilia.
Akaunti yake ina jina la @ Franciscus. Huu ni mtandao unaomwezesha Papa Fransisko kuwashirikisha vijana wanaojikita katika mitandao ya kijamii kuona baadhi ya picha, lengo ni kuvuka vikwazo vya lugha, ili kuwafikia watu wengi zaidi kwa njia ya lugha ya picha inayoweza kueleweka na watu wengi zaidi.
Katika ujumbe wake kwenye mitandao ya kijamii Papa amesema kuwa matumizi ya mtandao wa Instagram ni hija mpya anayopenda kuitumia ili kutembea na vijana katika njia ya huruma na upendo wa Mungu.

Baba Mtakatifu amezindua matumizi ya mtandao huu mjini Vatikani kwa kurusha picha yake ya kwanza inayomwonesha akisali.

Tukio hili limehudhuriwa na kushuhudiwa na Bwana Kevin Systrom, Mwakilishi mkazi na mwanzilishi mwenza wa mtandao wa Instagram pamoja na Monsinyo Lucio Adrian Ruiz, Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya Mawasiliano mjini Vatikani.

Mwenyekiti wa Sektretarieti ya Mawasiliano mjini Vatikani Monsinyo Dario ViganĂ²  amesema kuwa kitengo cha mawasiliano ya jamii katika Sektretarieti hii kitawajibika kuratibu akaunti ya Baba Mtakatifu katika mtandao wa kijamii wa Instagram, hasa wakati huu wa maadhimisho ya Mwaka Mtakatifu wa Jubilei ya huruma ya Mungu.

Mtandao huu utatumika pia kuwashirikisha vijana wa kizazi kipya picha na video fupi za Baba Mtakatifu Fransisko.

Ikumbukwe kuwa Papa ana akaunti ya Twita yenye zaidi ya watu Milioni 27 wanaomfuatilia, wakiwemo Rais wa Marekani Barack Obama na mwanamuziki Justin Bieber.


Chanzo: Radio Vatikani

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU