SHIGELA:"WAHALIFU TAFUTENI PA KUKIMBILIA"




MKUU mpya wa mkoa wa Tanga bwana Martin Shigela Amesema jambo analoanza nalo katika kazi yake mpya ni kukaa na kamati yake ya ulinzi na  usalama ili kupeana mikakati ya kuhakikisha wahalifu wote wanakamatwa na kufungwa jela.

Amewataka kuacha mara moja tabia hizo chafu kwani zinarudisha maendeleo nyuma kwa kuwanyima wananchi fursa za kujiletea maendeleo na taifa kwa ujumla.

Amekemea vikali baadhi ya uhalifu huo kuwa ni pamoja na ukwepaji kodi,biashara haramu na matumizi ya bandari bubu 19 ambazo imeelezwa zipo mkoani Tanga.

Ametoa onyo hilo wakati akikabidhiwa rasmi ofisi ya ukuu wa mkoa wa tanga kutoka kwa aliyekuwa mkuu wa mkoa huo Mwantumu Mahiza.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU