BEI JUU KWARESIMA:TANGA WALIA



Na VICTOR MKELLO WA RADIO HURUMA TANGA.
Wakazi wa mkoa wa Tanga wamelalamikia mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali unaozidi kuongezeka katika kipindi hiki cha kwaresima.
Akidhibitisha hayo mwenyekiti wa soko la Ngamiani   Mohamedi  Selemani amefafanua  kuwa chanzo cha kupandisha bei ya bidhaa katika soko  la Ngamiani ni kitendo  cha wao kuuziwa bidhaa kwa bei kubwa na hata kutozwa ushuru mkubwa ambapo  hupelekea  kupanda kwa bei kwani biashara kwa sasa ni ngumu na hasa katika kipindi hiki cha masika.
Hata hivyo baadhi ya wafanyabiashara katika soko hilo wameongelea changamoto wanazokutana nazo katika biashara zao hasa katika kupata wateja ndani ya soko  ambapo wamesema  kitendo cha serikali kuhamisha stendi ya mabasi kwenda kange kimesababisha kukosa wateja
Pia  baadhi ya wateja  akiwemo  Jeni  Msumari amesema suala la ongezeko la bei  hasa katika kipindi hiki cha kwaresima kwa kusema kwamba katika kipindi cha nyuma bidhaa zilikuwa zinauzwa kwa  bei  nafuu lakini wanashangaa  katika kipindi hiki bei zipo juu
Wafanyabiashara  hao  wamehitimisha kwa kuwaomba wananchi kuwa wavumilivu katika kipindi hiki cha mfumuko wa bei kwani ushuru wanaotonzwa  ni mkubwa na hii huwalazimu wao kuamua kuongeza bei katika bidhaa wanazouza  ili waweze kurudisha angalau  faida kidogo.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU