MAADHIMISHO MAZITO NA MATAKATIFU SANA YA PASAKA



Kanisa linaadhimisha Sherehe ya Pasaka kwa namna ya pekee sana katika Liturujia yake, wala hakuna sherehe nyingine yenye maadhimisho mazito kama hayo tunayoadhimisha Pasaka.
Uzito wa Maadhimisho ya Pasaka unatokana na matendo makubwa yanayoadhimishwa katika sherehe hiyo yaani mateso,kifo na hatimaye ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristu.Pamoja na kuadhimisha matendo hayo yaliyo kilele cha ukombozi,kanisa huadhimisha matendo makubwa ambayo Yesu aliyafanya kabla ya kuanza kwake mateso,ambayo ni kula Karamu ya mwisho na mitume wake na katika nafasi hiyo aliweka Sakramenti za Ekaristi,Daraja takatifu na amri ya mapendo.Kanisa huadhimisha matendo hayo makuu ya Pasaka katika Siku tatu kuu za Pasaka.
Licha ya kujiandaa kwa mfungo wa siku arobaini Juma moja kabla ya kuadhimisha ufufuko wa Bwana, kanisa linaanza rasmi kuadhimisha mateso ya Bwana katika Dominika ya Matawi ya Mateso ya Bwana.Kutokana na uzito wa kuadhimisha mateso na kifo cha Bwana, kanisa limetoa jina maalum kwa juma hilo kwamba ni Juma Kuu au Juma Takatifu.Juma hilo huitwa JumaKuu au Juma Takatifu kwa sababu kilele cha Juma hilo ni kuadhimisha SIKU TATU KUU ZA PASAKA.Siku tatu kuu za Pasaka huanza Alhamisi Kuu jioni kwa kuadhimisha Misa ya Karamu ya Bwana na kufikia kilele siku ya Dominika ya Pasaka.
 
Padri  Paul Chiwangu,TEC

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU