KIFO CHA MAMA ANGELICA;BENEDICT WA 16 ATOA NENO




Benedict wa 16 ametoa ujumbe juu ya kifo cha mama Angelica kilichotokea katika sikukuu ya pasaka akisema “NI ZAWADI
Askofu Mkuu Georg Ganswein ambaye ni katibu wa Benedict wa 16 ameuambia mtandao wa CNA juu ya ujumbe wa Papa mstaafu Benedict wa 16.
Mama Angelica ambaye ni mzaliwa wa Ohio,alikuwa mwanzilishi wa mtandao wa kikatoliki ulimwenguni wa EWTN huko nchini Marekani mwaka 1981.Baadaye ukaja kuwa mtandao mkubwa wa dini duniani.Amefariki dunia machi 27 katika sikukuu ya pasaka akiwa na miaka 92.
Kifo chake kimesababisha kumbukumbu kubwa maeneo mbalimbali duniani.
Huko Roma,mkuu wa sekretarieti ya mawasiliano Monsignor Dario Vigano ameahidi kufanya maombi maalum kwa kifo cha mama Angelica.Mapadri,walei na viongozi wa kidini Roma wanamwombea kwa ajili ya kifo chake.
Askofu Mkuu Joseph Kurtz wa Louisville na rais wa baraza la maaskofu Marekani amesema mama Angelica alikuwa mwanamke wa aina yake,muumini,mcha Mungu na moja kati ya waanzilishi wa vyombo vya habari.
Kristina Arriaga , mkurugenzi mtendaji wa Mfuko Becket wa Uhuru wa Kidini , amesema sista atakumbukwa kama " mfano wa kuigwa wa ujasiri na imani ."

CNA


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU