WAKATOLIKI WAASWA KUJITATHMINI KIPINDI CHA KWARESMA

n Na Agnes Shayo, Dar es Salaam
Waamini Wakatoliki nchini, wameaswa kujitafakari na kujitathmini ndani ya nafsi zao, kuhusiana na safari ya siku 40 za kipindi cha Kwaresma kisha kila mmoja kuona kwamba anahitaji huruma ya Mungu, ikiwa ni pamoja na kufanya mapinduzi ya Kiroho.
Wito huo umetolewa na Padri Francis Mtema, ambaye ni Makamu wa Askofu namba mbili wa Jimbo Kuu Katoliki Mwanza wakati akitoa homilia yake kwa waamini wa Parokia ya Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Jimbo Kuu Katoliki Mwanza wakati wa adhimisho la Ibada ya Misa Takatifu ya Jumatano ya Majivu.
Padri Mtema amesema kuwa amewakumbusha waamini kuwa kufunga si chakula tu, bali amewataka watambue kuwa vipo vitu mbalimbali vya kufunga katika kipindi hiki cha Kwaresma, ikiwa ni pamoja na yale yote yanayomuweka mkristo mbali na muumba wake, kama vile kutumia muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii, kwenye starehe, kutotimiza wajibu kazini, nyumbani au katika familia nk.
Wakati huo huo, Paroko wa Parokia ya Mikocheni Padri Adrea Mwekibindu, amezungumzia kuhusu kupakwa Majivu, akisisitiza kuwa, hii ni ishara ya kutakaswa/kusafishwa na ubaya wote wa dhambi ili kufanywa upya  na kumrudia Mungu, huku akiwasihi kila mmoja kushiriki toba hii katika kipindi hiki cha Kwaresma, pasipo kujali umri rangi wala muonekano, maana huruma ya Mungu iko wazi hivyo kila mmoja anaalikwa kuikimbilia.
Aidha amewakumbusha kuziishi nguzo kuu tatu ambazo ni muhimu kwa kila mmoja kuzifuata, huku akisema kuwa Mosi ni Sala, na kuwasaida wahitaji.
Kuhusu kufunga Padri Mwekibindu amesema kuwa kunawahusu wote wenye nguvu ili kuitisha miili yao, huku akiwataka kuwagawia wahitaji yale ambayo watakuwa wamejinyima wakati wote wa kwaresma. 
Safari ya Kwaresma imeanza siku ya Jumatano ya majivu na Itadumu kwa siku 40, ambapo Baraza la maaskofu limetoa ujumbe wenye Kauli Mbiu inayosema “Basi enendeni mkawafundishe mataifa yote kuwa wanafunzi wangi.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU