MAANDALIZI YA SIKU YA WANAWAKE YAPAMBA MOTO DODOMA

 Na Dotto Kwilasa, Dodoma.
KATIKA kuelekea maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani ambayo  hufanyika kila mwaka tarehe nane mwezi machi mwaka huu ,wananchi wa mkoa wa Dodoma hasa wanawake wametakiwa kujitokeza kwa wingi kusherekea siku hiyo muhimu kwao.
Kauli mbiu katika maadhisho hayo kwa mwaka huu ni ‘Kuelekea uchumi wa viwanda , Tuimarishe usawa wa jinsia ili kuwawezesha wanawake vijijini.’
Akizungumza hivi karibuni kwenye kikao cha kamati ya maandalizi ya Mkoa Makamu  Mwenyekiti wa kamati hiyo Rachel Mutoka amesema katika maadhisho hayo shughuli mbalimbali zitafanyika ikiwemo kutoa msaada wa kisheria, kupima afya kwa hiari na kupanda miti.
Mbali na hayo Mutoka amesema wanawake wanatakiwa kujitokeza ili kufanikisha maadhimisho hayo  na kuweza kupata msaada wa kisheria  ambao utawasaidia kutatua migogoro katika jamii ikiwemo ya  ndoa na mirathi.
Akifafanua zaidi alisema   mnamo tarehe mbili mwezi wa tatu  mwaka huu shughuli itakayofanyika ni kutembelea wodi ya wazazi katika  Hospitali  ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma na kufanya usafi.
“Tunatarajia kufanya mambo mbalimbali zaidi kwa maendeleo ya wanawake ambapo tarehe tano mwezi wa tatu tutatembelea kituo cha watoto yatima katika kijiji cha matumaini na gereza la wanawake Isanga na tarehe sita mwezi huo tutatembelea kituo cha wazee na Cheshire,” ameeleza.
Siku ya wanawake Duniani nchini Tanzania ilianza kuazimishwa  mwaka 1996 , ambapo maadhimisho hayo yamekuwa yakiandaliwa kitaifa na katika ngazi ya Mkoa.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU