WAHASIBU NA WASIMAMIZI WA MIRADI YA MAJIMBO KATOLIKI WAFUNDWA

Matukio mbalimbali yanayojiri katika ufunguzi wa semina inayowakutanisha wahasibu na wasimamizi wa miradi wa majimbo katoliki mbalimbali nchini, inayofanyika katika Kituo cha Kurasini-Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).

Semina hiyo inayolenga kuwajengea uwezo wa usimamizi wa fedha na miradi washiriki hao imeandaliwa na Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Katoliki Afrika Mashariki (AMECEA) kwa kushirikiana na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).
“Kama Kanisa tunapaswa kuwa mstari wa mbele kufuata sheria za kodi za nchi. Sheria na taratibu hizi siyo ngeni, zilikuwepo katika nchi yetu ila zilikuwa hazisimamiwi vizuri na kufuatiliwa” Katibu Mkuu wa TEC Padri Raymond Saba.

“Semina hii iwasaidie na ninyi mkaandae semina kama hizi huko majimboni. Tukumbuke kuwa mambo haya ya fedha na miradi yanagusa taasisi ambazo majimboni kwetu ziko nyingi. Kwa hiyo sisi tunalo jukumu la kufikisha ujuzi huu katika ngazi ya chini kabisa, ikiwezekana hata katika jumuiya ndogo ndogo” Padri Chrisantus Ndaga, Naibu Katibu Mkuu AMECEA. (Na Pascal Mwanache)







Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU