Mbaroni kwa kuteketeza mabweni ya seminari ya St.Mary’s,Mbeya

n Na Thompson Mpanji, Mbeya
Baada ya uchunguzi wa Seminary Ndogo ya St. Mary’s Mbeya pamoja na polisi kuhusu chanzo cha moto ulioteketeza mabweni mawili  ya Seminari hiyo kwa nyakati tofauti mtuhumiwa wa tukio hilo amekamatwa na kutiwa mbaroni.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili zinasema kuwa baada ya matukio yote mawili Uongozi wa shule ya St.Mary’s Mbalizi uliamua kuimarisha ulinzi  shirikishi kwa wanafunzi wenyewe kuwekeana zamu  na hivyo kufanikiwa kuwanasa vijana wanne   wanaodaiwa kukutwa na dumu la mafuta yanayodhaniwa kuwa ni petroli majira ya usiku  wakitaka kuchoma moto majengo mengine wakati wanafunzi wakiwa wamelala.
Aidha taarifa hizo zinasema kuwa vijana watatu walifanikiwa kutoroka kusikojulikana na kubakia na kijana mmoja ambaye  ametiwa mbaroni.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya,Naibu Kamishna Mpinga amethibitisha kukamatwa kwa kijana huyo (jina limehifadhiwa kwa sababu za kiuchunguzi)  mwenye umri wa miaka 12 ambaye  alikuwa ni mwanafunzi wa kidato cha awali katika seminari hiyo siku ya jumamosi Februari,3,2018 na baada ya mahojiano amekiri kuhusika kutenda matukio yote mawili ya kuteketea kwa  mabweni hayo.
“Tumefanikiwa kumkamata kijana  mmoja  siku ya jumamosi  alikuwa mwanafunzi wa pre form one katika shule hiyo ambaye kwa sababu  za kiuchunguzi na kiusalama  jina linahifadhiwa  na amekiri kuhusika katika matukio yote mawili kutokana na shinikizo la mtu mmoja aliyemtishia kuwa asipotekeleza uhalifu huo atamkata na mapanga,kwa hiyo tunamshikilia na tunaendelea na uchunguzi zaidi”amehitimisha Kamanda Mpinga.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU