UJUMBE WA PAPA FRANSISKO WA 52 SIKU YA MAWASILIANO DUNIANI 2018

SIKU ya Upashanaji wa habari huadhimishwa kila mwaka katika maadhimisho ya sherehe za Kupaa Bwana Mbinguni ambapo mwaka huu itafanyika Mei 13. Ujumbe huu unaongozwa na kauli mbiu “UKweli utawawekeni huru: Habari potofu (Fake news) na uandishi wa amani”
Katika ujumbe wa Baba Mtakatifu, anasema, katika mpango wa Mungu, mawasiliano ya binadamu ni muhimu katika kuishi umoja. Kama Binadamu ni sura na mfano wa Mungu ana uwezo wa kujieleza na kushirikishana ukweli, uzuri na wema. Ana uwezo wa kusimulia uzoefu wake binafsi katika dunia na kujenga kumbukumbu ya uelewa wa matukio.
Lakini binadamu kwa kuongozwa na ukiburi wake na ubinafsi hawezi kutoa mawasiliano mema kama inavyojionesha katika matukio ya Biblia katika historia ya Kaini na Abeli, hata tukio la Mnara wa Babeli. (Mw 4,1-16; 11,1-9).
Kubadilisha ukweli ni dalili ya kawaida ya upotofu ambayo mtu hufanya binafsi na kwa pamoja. Kinyume chake katika imani kwa mantiki ya Mungu, mawasiliano ni sehemu ya kuelezea uwajibikaji kwa kutafuta ukweli na ujenzi wa wema. Leo hii lakini katika dhana ya mawasiliano, daima inayojionesha wepesi na ndani ya mfumo wa kidigitali, kwani yanaonekana matukio mengi ya habari za uwongo ziitwazo fake news.
Kulingana na haja hiyo Baba Mtakatifu anapendelea kutoa ujumbe wa mada ya ukweli ambayo anasema, mara nyingi watangulizi wake kuanzia mwenye heri Paulo VI (katika ujumbe wa mwaka 1972; ilikukuwa na mada ya “Mawasiliano ya kijamii katika huduma ya ukweli”).
‘Fake news’ ni jambo nyeti linalojadiliwa na kitu cha mjadala! Kwa ujumla unajikita kutazama kwa kina juu ya utoaji wa habari za upotofu katika mitandao ‘Online’ au katika mitandao kijamii, na ya utamaduni asili. Kwa maelezo hayo ni kusema kuwa, ni habari za uwongo, zisizo na msingi kwa uwepo wake; zenye nia ya kutaka kudanganya hadi wasomaji na watazamajiwake. Usambazaji wa fake news unaweza kujibu lengo walilokusudia, kwa kushawishi uchaguzi wa kisiasa na kukuza mapato yao kiuchumi.
Ufanisi wa fake news unajitokeza awali ya yote mahali ambapo wao wanaigiza kwa asili yao yaani uwezo wa kutaka kuonekana na kusifika. Na hatua ya pili, habari za uwongo ambazo zinafanana, zinavutia, kwa maana ya kupendwa na kuchukuliwa makini na walengwa. Kwa kuwa na uwezo wao wa kulaghai, hufanya marudio ambayo yanasambaa kwa haraka ndani ya maisha ya kijamii na kuwatumia wenye hisia rahisi, kuziamsha kwa haraka, kwa mfano wa kuleta wasiwasi,dharau,hasira na kuchanganyikiwa.
Usambazaji wa habari za uongo unatumia kwa ujanja mitandao ya kijamii na kwa mantiki ya kuhakikisha inafanya kazi. Kwa namna hiyo mambo msingi yaliyomo ndani ya habari za uongo, pamoja na ukosefu wa msingi, unapata mwonekano hadi kufikia mamlaka husika kukosa uhalifu wake. 
Baba Mtakatifu anazidi kufafanua kuwa, matatizo yanayoonesha kusambaa kwa habari za uongo yametokana na kwamba watu wengi mara nyingi wako katika mazingira ya kidigitali ya pamoja, ambayo ni rahisi kupitia mantiki nyingi na maoni tofauti.
Na matokeo ya mantiki ya habari potofu, ni kwamba, badala ya kukabiliana vema na vyanzo vingine vya habari, jambo ambalo linaweza kuleta uchanya wa mjadala na kufungua mazungumzo ya ujenzi, inageuka kuwa hatari hata bila utashi wa wadau wake ambao usambaza maoni ya uwongo na ushahidi.
Tishio la habari potofu ni ung’oaji wa mzizi wa mwingine na uwepo wake unakuwa kama adui, hata kuwa shetani ambaye anaweza kutoa ushahidi wa migogoro ya uwongo; ndivyo habari za uwongo zinavyjionesha uwepo wake hasa tabia ya kutojali, anasisitiza Baba Mtakatifu Fransisko.
2.Ni jinsi gani ya kutambua?: Baba Mtakatifu Fransisko anasema, hakuna hata mmoja anayeweza kusamehemewa jukumu la kupinga uongo huo! Lakini pia anatambua kwamba, si kazi rahisi, kwa maana usambazaji wa uwongo unapitia katika mazungumzo mengi ambayo yanasambaratika kichini chini pia udanganyifu wake mara nyingi ni wenye mfumo wa kisirisiri.
Kwa njia hiyo Baba Mtakatifu anasistiza kwamba iwapo inawezekana basi kuanzishwa mafundisho ambayo yanajikita hasa kuchukua hatua ya kusoma na kuchunguza mantiki hiyo ya mawasiliano. Ni mafundisho ya dhati ili kuweza kuacha tabia ya usambazaji wake; kuwa na utambuzi kwamba habari zenye uwongo na kwa maana hiyo, kuwa na wadau wa kueleza wazi wahusika.
Licha ya hatua hiyo ya mafunzo ni pamoja na ile ya kuanzisha taasisi na kisheria ambazo zinajikita kwa kina katika kusitisha matukio hayo, kama vile hata taaluma ya hali ya juu ya kiteknolojia na makampuni ya mitambo ya kutafuta dhana mpya ya kuhakiki na kuwatambua wahusika wanaojificha nyuma ya milioni ya picha za kidigital.
Hata hivyo Baba Mtakatifu anabainisha kuwa, uzuiaji na mtambo wa ugunduzi wa habari za uwongo, awali ya yote unahitaji hata umakini wa kina na mang’amuzi. Ki ukweli ili kuweza kuwagundua, Baba Mtakatifu anaongeza kuna kile  ambacho chaweza kuelezwa kwamba ni mantiki ya nyoka,  mwenye uwezo wa kujificha mahali popote ili aweze kuuma.
Inahitaji mkakati wa nyoka mjanja ambaye anatajwa katika Kitabu cha Mwanzo, yeye alikuwa wa kwanza kumdanganya binadamu ikawa ndiyo fake news ya kwanza  (Mw 3,1-15), baadaye ikasababisha majanga yote ya dhambi hadi kufikia  mauaji ya kwanza,  Kitabu cha mwanzo sura ya 4, na  hata katika idadi kubwa ya mitindo ya ubaya dhidi ya Mungu, jirani, jamii na kazi ya uumbaji.
Mkakati wa uwezo huyo aitwaye  baba wa uwongo kama Injili ya Yohane ilielezavyo, ( Yh 8,44) ni mkakati wa kujibuluza,wa hatari ya ulaghai kwani anatengeneza njia katika moyo wa binadamu kwa kutumia  maelezo mengi ya uwongo na kutamanisha. Hayo yanajionesha katika maelezo ya dhambi ya asili, kwani, mshawishi alimkaribia mwanamke na kujifanya kama rafiki akionesha kujali wema wake, akaanza mazungumzo utafikiri ya kweli, lakini yalikuwa ukweli nusu nusu:“Ni kweli Mungu alisema: mwaweza kula matunda ya mti wowote katika bustani, lakini matunda ya mti wa ujuzi wa wema na mabaya msile.... (Mw2,17).
Mwanamke alijibu na kuelezea nyoka, lakini kwa kutaka kumfafanulia zaidi: “Twaweza kula matunda ya mti wowote bustanini, lakini matunda yaliyoko katikati ya bustani msiuguse ili tusije tukafa (Mw 3,2)
Baba Mtakatifu anafafanua, Jibu hili la mwanamke  linatolewa kama vile la kisheria na lenye ugumu: kwa maana alionesha imani kwa mshawishi na kujiachia avutiwe naye, ndiyo maana mlaghai  akabadilisha majibu hayo, akamwambia mwanamke “hamtakufa (Mw 3,4) “kwa maana alisema hivyo kwasababu anajua kwamba mkila matunda ya mti huo mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu mkijua mema na mabaya”! Mw 3,5).
Kwa njia hiyo, Baba Mtakatifu anasema, nyoka alikuwa amefanya kazi yake ya kumwondoa mwanamke katika amri ya Mungu iliyokuwa ya wema na kufuata ushawishi wa adui shetani kwa maana “mwanamke huyo aliona kuwa mti huo ni mzuri kwa chakula na wavutia macho”… (Mw 3,6).

Baba Mtakatifu anasisitiza, katika matukio hayo ya biblia yanaonesha wazi hali halisi na msingi katika kuthibitisha na kuonesha juu ya utoaji wa habari za uongo kwamba, hakuna maelezo ya kutofahamika; kinyume chake, kuamini uongo huzalisha matokeo mabaya. Hata upotofu wa ukweli unaoonekana kidogo unaweza kuwa na athari za hatari.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU