Oktoba 7 kilele jubilei miaka 150 ya uinjilishaji

n  Na Pascal Mwanache, Dar
HATIMAYE ratiba ya kilele cha Jubilei ya Miaka 150 ya Uinjilishaji Tanzania Bara imetolewa, huku siku ya kilele ikitajwa kuwa ni Oktoba 7, 2018 na maadhimisho hayo yanatarajiwa kufanyika Bagamoyo.
Akitoa ratiba hiyo kama ilivyopendekezwa na Maaskofu, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Padri Raymond Saba amesema kuwa katika Mkutano wa Maaskofu wamepitisha siku ya Oktoba 7 kuwa kilele cha jubilei hiyo.
“Kwa hiyo tunategemea watu kutoka majimbo mbalimbali wawasili Bagamoyo Oktoba 5, huku Oktoba 6 ikiwa ni siku maalum kwa ajili ya semina, maungamo na kuabudu Ekaristi. Kilele kitakuwa Oktoba 7 na Oktoba 8 watu wataanza kurejea nyumbani kwao” ameeleza Padri Saba wakati akiwasilisha ratiba hiyo kwa wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Jubilei hiyo.
Aidha Padri Saba amesema kuwa Maaskofu wameichagua na kuipitisha Dominika ya nne ya Kwaresima kuwa ni siku maalum ya uchangiaji wa maandalizi ya jubilei hiyo, ambapo sadaka itakayotolewa katika makanisa yote nchini itakuwa ni mchango kwa ajili ya maandalizi ya jubilei hiyo.
Kamati ya Maandalizi ya Jubilei hiyo imeanza kukutana na kupeana majukumu mbalimbali yenye lengo la kufanikisha jubilei hiyo.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU