JUMAPILI YA 4 YA KWARESIMA SIKU YA KUCHANGIA JUBILEI YA MIAKA 150 YA UINJILISHAJI

Na Sarah Pelaji, Dar es Salaam
wAKATI Kanisa Katoliki nchini linajiandaa kushurehekea Jubilei ya miaka 150 ya Uinjilishaji Tanzania Bara,  Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) limetangaza kuwa, Dominika ya 4 ya Kwaresima mwaka huu, yaani  11 Machi 2018, sadaka zote za Misa Takatifu za siku hiyo kwa nchi nzima (vigango, parokia, Majimbo yote Tz) zitakusanywa na kuwasilishwa TEC ili kusaidia maandalizi ya maadhimisho ya Jubilei hiyo.
Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam Mhashamu Euzebius Nzigilwa amesema kuwa hayo ni maazimiao ya  Mkutano wa TEC wa Januari 25 mwaka huu .
Kauli mbiu ya Jubilei hiyo ni ‘Miaka 150 ya Uinjilishaji, Furaha ya Injili.’
“Machi 11 mwaka huu yaani Jumapili ya 4 ya kwaresima (Laetare) hakutakuwa na michango mingine yoyote ya kiparokia siku hiyo. Sadaka yote ya kwanza na ya pili ikusanywe na kupelekwa Jimboni ili iweze kuwasilishwa Taifani.
Pia jumapili hiyo itumike kwa ajili ya kuhamasisha  waamini juu ya maadhimisho ya Jubilei hiyo ambayo kilele chake ni Oktoba 7 mwaka huu huko Bagamoyo badala ya Oktoba 2 mwaka huu kama ilivyokuwa imetangazwa awali,” ameeleza Askofu Nzigilwa.
Aidha ameeleza kuwa, Mapadri, Watawa na Waamini wote wanaalikwa kujiandaa na kushiriki kwa ibada na hija; na kwa hali na mali katika maadhimisho ya Jubilei hiyo katika ngazi ya Parokia, Jimbo, Kanda (Metropolitan) na Kitaifa.
Aidha, Makundi mbalimbali ya Familia ya Mungu yanatakiwa kufanya maadhimisho ya Jubilei hiyo katika ngazi ya Jimbo katika muda tofauti.
Vijana wanapaswa kufanya  maadhimisho yao Machi 25 mwaka huu, watawa April 8 mwaka huu, Wazee April 15 mwaka huu na Walei Mei 20 mwaka huu.
Aidha watoto wanapaswa kufanya maadhimisho yao Juni 3 mwaka huu, Jumuiya ndogondogo Julai 8 mwaka huu, Vyama vya Kitume Agosti 12 maka huu na Mapadri Septemba 2 mwaka huu ndipo makundi hayo yote yataungana kwenye kilele Oktoba 7 mwaka huu Bagamoyo.
Tarehe za maadhimisho hayo ya makundi ni kwa nchi nzima.
 Waamini wanahimizwa kusali Sala Maalum ya Jubilei katika parokia, jumuiya na katika vyama vyao vya kitume.
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amesisitiza waamini wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam  kushiriki vema na kufanya utekelezaji wa maagizo hayo ili kufanikisha jubilee hiyo.
Amewaasa hasa wale walengwa wa kufanya maadhimisho ya makundi maalumu, walezi na viongozi wao wamuone mapema iwezekanavyo kueleza namna watakavyoshiriki pamoja na mapendekezo ya mahali yatakapofanyika maadhimisho hayo.

Kamati Kuu ya maandaliazi ya Jubilei hiyo kitaifa imewasihi maparoko kuhimiza waamini wao juu ya Jubilei hiyo na kushiriki kwa wingi katika maadhimisho ya makundi na maadhimisho ya kilele huko Bagamoyo Oktoba 7 mwaka huu.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU