Askofu Minde ahimiza nidhamu na utii kwa watawa

Na  Patrick Mabula, Kahama.
Askofu wa Jimbo Katoliki Kahama Mhashamu Ludovick Minde amewaasa watawa kuwa na nidhamu  kwa Kanisa  katika utume  wao.
Amesema hayo katika Ibada ya Misa Takatifu ya kusherehekea Jubilei ya miaka 25 ya kumshukuru Mungu kwa Masista  wanne wa  shirika la Mtakatifu Fransisko wa Asizi  na mmoja aliyekuwa  akiweka  nadhiri za daima iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Luka Mwinjili jimboni humo.
“Hakuna upadri au utawa bila Kanisa, hilo lazima lifahamike wazi. Lazima wote tuwe na utii na nidhamu kwa sababu miito yote ni kwa ajili ya Kanisa katika kumtumikia Mungu na si vinginevyo.
 Katika maisha ya wito kuna muunganiko kati ya Kanisa na Yesu Kristo. Hivyo watawa waone muunganiko huo katika utume wao ili ung’are kwa matendo na mwenendo wao,” amesema.
 Askofu Minde amewasihi watawa kuishi maisha ya neema ili uwavute wengine kuingia kuwa  wito huo wakijiunganisha na Kanisa na Kristo.
 Aidha watawa wakumbuke kuwa wana wajibu wa kujikita katika utume wao kwa Kanisa na kwa jimbo bila  makandokando.  
Amewaasa waamini kuwaombea Maaskofu, Mapadri na Watawa ili waweze kuwa watumishi wema na kuwavuta watu kuingia katika miito ya upadri na utawa Kanisa lipate watumishi.
Kwa upande wake Msimamizi wa Watawa wa Jimbo Katoliki Kahama Padri David Mwangu amesema kuwa, watawa ni zawadi ya Mungu kwa Kanisa , wajifunze kusikia sauti ya Mungu na kujitoa kwa kumtumikia katika Kanisa lake mahalia.
Watawa waliyo sherehekea miaka 25 ya utawa ni Mama Mkuu wa Shirika hilo Frasisko wa Asizi, Sista Bernadetta Musibimana, Sista Liberatha Mukantwari, Sista Christina Kasana , Sista Esther Nyawile na aliyeweka nadhiri za daima ni Sista Bertha Manyanda.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU