Mtawa afariki Kahama




Na  Patrick Mabula , Kahama.
Jimbo Katoliki Kahama limepatwa na simazi baada ya  kufiwa na Sista Elizabert   wa shirika la Wamisionari wa Masista Wabenediktine aliyefariki   hivi karibuni baada  gari yake aina ya Land Cruser kuanguka  katika   eneo  la Kanegere alipokuwa katika  kazi  zake za  kitume .
Akizungumza katika Misa Takatifu ya kumuombea Marehemu Sista Elizebert, Askofu wa Jimbo Katoliki Kahama Mhashamu Ludovick Minde amesema kuwa, kifo hicho wamekipokea kwa mshtuko, simanzi na majonzi .
“Sista Elizabert alimpenda Yesu , alimpenda Mungu na hakuacha njia ya utume wake katika Kanisa.
  Kifo chake kimenisikitisha kwasababu amefariki ghafla lakini tunapaswa kumshukuru Mungu kwa zawadi ya sista  huyu aliyekuwa anajitoa katika utume wake kwa  kumtumikia Mungu na waumini wote bila ubaguzi  na alilipenda Kanisa,” Amesema Askofu Minde katika Misa Takatifu ya kumuombea iliyofanyika katika Kanisa la Ekaristi  Takatifu Parokia ya Kabuhima.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU