Kazi ya UWAKA ni kuimarisha familia, Kanisa-Askofu Chengula

Na Thompson Mpanji,Mbeya
ASKOFU  Evarist   Chengula(IMC) wa Jimbo Katoliki Mbeya  amewaalika Umoja wa Wanaume Kanisa Katoliki(UWAKA) kuwa watu wa msamaha kwa wenzi wao na chachu  ya miito  kwa ajili ya Kanisa .
Askofu  Chengula  ametoa wito huo wakati  wa Ibada  ya Misa Takatifu ya Siku kuu ya Mt.Yoseph Mfanyakazi iliyoambana  na uzinduzi wa Umoja wa wanaume katrika Parokia ya Ruanda.
 Amesisitiza kuwa, vyama vya kitume ndiyo mishipa ya damu  ya ukombozi katika Parokia yeyote .
“Ninawaomba sana mtumie nafasi hii ya kusaidiana  ili kudumusha umoja huu ambao ninaamini utaleta mageuzi na mabadiliko kuanzia mtu binafsi, familia zenu, jumuiya ndogondogo na parokia.
Uhai wa chama chenu utategemea kwanza juhudi zenu nyie wanaume mkishirikiana na akina mama.
Muwe chachu ya miito katika familia zenu, jumuiya na parokia.
Pia muimarishe familia zenu kwa fadhila ya msamaha. Muwasamehe wake zenu, watoto na kuwa wapatanishi katika Kanisa,” amesisitiza .
 Amesema kuwa endapo  Uwaka itafanya kazi ipasavyo itasaidia kwa asilimia kubwa kuondoa ama kumaliza kabisa changamoto za wazazi kuwafukuza watoto  wanaokimbilia mitaani.


Comments

  1. Asante sana. Tunatumia Elimu hii katika jumuiya kanda

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU