Padri awasisitiza waamini kuzithamini Kumbukumbu za Watakatifu

n Na Philipo Josephat, DSM

WAKRISTO  wote  wametakiwa kuzipa  umuhimu  na  kuzisherehekea   sikukuu  mbalimbali za  watakatifu  wa  Kanisa  ikiwemo  ile  ya Bikira  Maria  kupalizwa  mbinguni.
       Wakiongea  wakati  wa kusherekea  sikukuu  ya  kupalizwa   Bikira  Maria mbinguni, baadhi  ya  wanajumuiya  ya  Bikira  Maria Mpalizwa  wa  Mbinguni wamesema  kila  mkristo  anapaswa  kujua wajibu  wake  wa  sala  kwa  kumuomba Bikira Maria  awaombee  kwa  mwanae  Yesu.
Mwenyekiti  wa Jumuiya  hiyo toka  parokia  ya Kimbiji Dar  es  salaam    Joseph  Kusandika   amewataka  wakristo  kupeleka  sala  zao  kwa  Bikira  Maria  ili  wapate  amani  ambayo   italeta  mwanga  mpya  ndani  ya  familia  na jumuiya  zote.
Paroko  msaidizi wa parokia  ya  Kimbiji  padri  Justus   Lugayimkam aliyeongoza Misa hiyo ameeleza juu ya mwanzo  wa  sikukuu  ya  kupalizwa  Bikira  Maria  mbinguni. “Sikukuu  ya  kupalizwa  mbinguni  Bikira  Maria ilitangazwa  rasmi  mnamo  mwaka  1950  na  Papa  Pius  wa  kumi  na  mbili,  na  mnamo  karne  ya  6,550 BK  ilijulikana  kama  sikukuu ya  Domisiyo  wakati  mnamo  karne  7-8  ikajulikana  kuwa  sikukuu  ya  Somisiyo,  kuanzia  karne  ya 8-21  na  hadi leo  inajulikana  kuwa  ni  sikukuu  ya  kupalizwa  Bikira  Maria  mbinguni,” amesema  padri Lugayimkam.
Aidha  padre Lugayimkam ameongeza  kuwa  zipo   sababu   kuu  nne  zinazoeleza kupalizwa  kwa  Bikira  Maria  mbinguni, sababu  ya  kwanza  ni  kwamba  Bikira  Maria  alikingiwa  dhambi  ya  asili,  ya  pili  Bikira  Maria  alidumu katrika  ubikira  wake,  tatu  Bikira  Maria  ni Mama  wa  Mungu na  ya mwisho ni ukaribu  wake  na mwanaye   Yesu  Kristo.
Wakati  huohuo  wakristo wote  wanatakiwa kuishika, kuitetea  imani  bila  kujali  adha  au  matatizo ambayo  yatawapata.
Hayo  yamesemwa  hivi karibuni katika kigango  cha  Mbutu  Kigamboni  Kimbiji  Dar   es  salaam   na  padri  Justus.
“Mkristo  anapoiacha  imani moja  kwa  moja  anaingia  kwenye  matatizo  makubwa yatakayomtenga  na  Mungu, kilicho  mfanya Petro kuzama  kwenye  bahari  wakati  Yesu  alipomuita atembee  juu  ya  maji  ni  kukosa  imani, hofu na  mashaka  ya upepo  uliokuwa  ukivuma  baharini na  kusababisha  kuanza  kuomba  msaada  kwa  Yesu amuokoe. Katika  sura  hiyo  waamini  wanapaswa  kutambua  kuwa   kwa  sayansi  ya mwanadamu  ni vigumu  kutembea  juu  ya maji, lakini  ndiye  mwanasayansi  namba moja  katika  maisha  yetu  yote ,hivyo  inampasa kila  muamini  kumfuata  Kristo  na  kuilinda  imani  itupatiayo  wokovu.”


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU