Wito ni kazi ya Mungu siyo mwanadamu-Ask. Kinyaiya

Na Rodrick Minja, Dodoma

ASKOFU Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma Mhashamu Beatus Kinyaiya amesema kuwa wito anaoitiwa mwanadamu yeyote siyo wake  bali ni wito unaotoka kwa Mwenyezi Mungu.
Ameyasema hayo wakati wa adhimisho la misa takatifu ya utoaji wa daraja takatifu la ushemasi kwa mafrateri Dickson Komba na Justine Bonifasi wa Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu, iliyofanyika katika Parokia Bikira Maria Mama wa Damu azizi ya Yesu Kisasa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma.
Amesema kuwa mtu anapoitwa katika wito fulani na Mungu anapaswa kuitikia hima ‘ndio’ mpaka tamati na siyo kukatiza akiwa njiani.
Askofu Kinyaiya amesema kuwa Mungu anajua aina ya watu anaowachagua katika kuingia katika wito mtakatifu.
“Mfano Yesu alimchukua Petro na kuwa mfuasi wake lakini siku Yesu anateswa Petro alimkana kuwa hamfahamu, hivyo msiwe kama Petro nyie simameni katika njia iliyo bora mliyoichagua” amesema Askofu Kinyaiya.
Hata hivyo amewataka kuhakikisha katika maisha ya wito walioitiwa katu wasikubali kuukana wito huo, bali waukumbatie katika hali zote watakazokumbana nazo katika utume wao.
Aidha Askofu Kinyaiya amewataka waamini mahalia kuwasaidia mashemasi hao katika wito wao pasi kuwaingiza kwenye vishawishi vitakavyowakwaza katika utume wao.
Amesema kuwa kila mmoja wetu anao udhaifu wake lakini katu usikubali kuuonyesha kwa watu wengine kuwa thabiti katika utume wako na kuweni jasiri na kila mlifanyalo mtangulizeni Mungu mbele.
Amesema kuwa kama wao walivyochaguliwa katika kundi la watu wanapaswa kuonyesha mfano wa kuigwa na katu wasiwe vikwazo bali wawe ni daraja ambalo litawavusha watu kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa hali ya amani na upendo.
“Mmekabidhiwa na kutumwa mkawe wavuvi, wavuvi ni watu ambao wanavua samaki, ila nyie samaki wenu ni kundi kubwa la kondoo waliokabidhiwa na mwenyezi mungu amablo ni waamini mahalia hivyo wawafundishe yale wanayowapasa hususani katika kulihubiri neno la mungu.” Aliongeza.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU