DC Songwe apongeza utendaji wa Askofu Nyaisonga

Na Thompson Mpanji, Songwe

MKUU wa Wilaya  ya Songwe,Samwel Jeremiah  amemuelezea Askofu Mkuu  wa Jimbo Kuu Katoliki la Mbeya,Mhashamu Gervas Nyaisonga  kuwa ni mtu wa aina yake ambaye  amejawa hekima na busara katika uchungaji wake.
Mkuu huyo wa Wilaya amesema hayo  alipokuwa mgeni rasmi  katika mahafali  ya tisa ya kuwaaga  wahitimu  wa mafunzo  ya Uuguzi na Ukunga  katika ngazi ya stashahada katika Chuo cha Mwambani, kilichopo Kata ya Mkwajuni, wilaya ya Songwe, mkoani Songwe.
 “Kwa kweli nimemshangaa  na kumuona ni kiongozi wa ajabu na nilikuwa nikimsikia na leo nimejionea nilipoambiwa kuwa yeye Askofu Mkuu  amekataa kuwa mgeni rasmi na kupendekeza lazima awe Kiongozi wa Serikali...
Nilijiuliza sana kwamba kwanini Baba Askofu amefanya hivyo...nikasema Baba amejawa na unyenyekevu, hekima na busara  za pekee,”anasema Mkuu wa wilaya hiyo na kuongeza;
“Niseme tu Baba Askofu leo umenipa heshima kubwa sana  kuwa mgeni rasmi wa tukio hili . mahafali ya leo yakabadilishe  maisha ya wauguzi  na wakunga wote, nimeambiwa  kuwa  chuo  hiki.”
Hata hivyo amewataka   wahitimu kuondoa hofu  juu ya ajira   kwani serikali ya awamu ya tano inatoa kipaumbele  kwa sekta ya afya.
“Niwaambie tu kuwa  kuna hospitali zaidi ya 67  na vituo vya afya zaidi ya 350 vinajengwa nchi nzima vyo hivi  vikikamilika vinahitaji  wahitimu kama ninyi mkafanye kazi kwa kuzingatia maadili na kuliletea  sifa Kanisa,” amesema.
 Kwa upande wake Askofu Mkuu Gervasi Nyaisonga amewasihi  wahitimu  hao ambao  wameapa kiapo cha utii  kama alivoapa mwanzilishi wa fani ya uuguzi duniani Florence Nightngale kuwa  kielelezo ya maisha yao katika utume  wao  na wanapoishi.
 “Naomba kiapo kile  kiwe kwa vitendo kule muendako,mkafanye kazi kama mlivyofundishwa kwa bidii, kwa uaminifu na kwa umakini wa hali ya juu ukumbuke kuwa unayemhudumia ni binadamu kama wewe , fanya kazi huku ukimuhusisha Mungu katika kazi zako,” amesema Askofu Nyaisonga.
Askofu Nyaisonga amesema Serikali inayo mkono mrefu, inayo nguvu na ndiyo imepewa dhamana na  Mwenyezi Mungu kusimamia rasilimali za Nchi,kwa hali hiyo hatuna namna na  hatuwezi kufanya chochote bila kuitegemea serikali vinginevyo tutaendelea kushirikiana nanyi na hatutachoka kuja kuwaona kuomba ushauri na misada ya namna mbalimbali.
 Kwa upande  wake Muuguzi Mkuu wa Mkoa wa Songwe, victoria Mwakigili alipigilia msumari kuhusu suala la mavazi ambayo wanapaswa kuvaa  wauguzi ikiwemo kutumia lugha nzuri kwa wagonjwa.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU