MASOMO YA MISA, APRILI 25, 2018

MASOMO YA MISA, APRILI 25, 2018
JUMA LA 4 LA PASAKA, JUMATANO
SIKUKUU YA MTAKATIFU MARKO, MWINJILI


SOMO 1
1 Pet 5: 5-14

Ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema. Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu. Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze. Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika ¡mani, mkijua ya kuwa mateso yale yaie yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani. Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika «risto, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawatengeneza, na kuwathibitisha, na kuwatia nguvu. Uweza una yeye hata milele na milele. Amina.

Kwa mkono wa Silwano, ndugu mwaminifu kama nionavyo, nimewaandikia kwa maneno machache, kuonya na kushuhudia ya kuwa hii ndiyo neema ya kweli ya Mungu. Simameni imara katika hiyo. Mwenzenu mteule hapa Babeli awasalimu, na Marko mwanangu. Salimianeni kwa busu la upendo. Amani na iwe kwenu — nyote, mlio katika Kristo. Amina.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 89: 1-2, 5-6, 15-16

(K) Fadhili zako nitaziimba milele, Ee Bwana
au: Alleluya

Fadhili za Bwana nitaziimba milele;
kwa kinywa changu nitavijulisha vizazi vyote uaminifu wako.
Maana nimesema, fadhili zitajengwa milele;
katika mbingu utauthibitisha uaminifu wako. (K)

Ee Bwana, mbingu zitayasifu maajabu yako,
uaminifu wako katika kusanyiko la watakatifu.
Maana ni nani katika mbingu awezaye kulinganishwa na Bwana?
Ni nani afananaye na Bwana miongoni mwa malaika? (K)

Heri watu wale waijuao sauti ya shangwe,
Ee Bwana, huenenda katika nuru ya uso wako.
Kwa jina lako hufurahi mchana kutwa,
Na kwa haki yako hutukuzwa. (K)

SHANGILIO
1 Kor. 1:23-24

Aleluya, aleluya,
Sisi tunamhubiri Kristu, aliyesulibiwa, ni nguvu na hekima ya Mungu.
Aleluya.

INJILI
Mk 16: 15-20

Yesu aliwaambia wale Kumi na mmoja, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hatawakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya. Basi Bwana Yesu, baada ya kusema nao, akachukuliwa juu mbinguni, akaketi mkono wa kuume wa Mungu. Nao wale wakatoka, wakahubiri kotekote, Bwana akitenda kazi pamoja nao, na ulithibitisha lile neno kwa ishara zilizofuatana nalo.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU